Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Zahor Mohamed Haji

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwera

Primary Question

MHE. ZAHOR MOHAMMED HAJI aliuliza: - Je, Serikali inachukua hatua gani kwa viongozi wanaowanyima wananchi kwa makusudi haki yao ya kuwa wanufaika wa TASAF?

Supplementary Question 1

MHE. ZAHOR MOHAMMED HAJI: Mheshimiwa Spika, naomba niishukuru Serikali kwa majibu yake mazuri, lakini naomba niulize maswali mawili ya nyongeza; la kwanza, je, Serikali inatambua kwamba tabia hii inafanyika katika jimbo langu?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; Je, Serikali sasa iko tayari kulifanyia kazi hii ili kuondokana na tatizo hili kwa wananchi?

Name

Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI
WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba Serikali inatambua juu ya tabia za baadhi ya viongozi au wananchi wanaoshiriki katika kuhakikisha kwamba wanawanyima watu haki zao. Nataka nimwakikishie Mheshimiwa Mbunge, kwamba kwa kutambua hilo Serikali imejidhatiti kuhakikishi kwamba inachukua hatua zote husika na pale inapotokea wananchi wanashindwa kwenda kushtaki basi na sisi pia kama wawakilishi wa wananchi tunaruhusiwa kufikisha vilio katika ofisi hizo mbili ikiwemo mkurugenzi na ofisi ya makamu wa pili wa Rais kama nilivyoeleza.

Mheshimiwa Spika, kuhusu swali la pili, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali itaendelea kuhakikisha kwamba haki za watu wote wanaostahiki kuingia katika mfuko wa TASAF zinapatikana.

Name

Miraji Jumanne Mtaturu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mashariki

Primary Question

MHE. ZAHOR MOHAMMED HAJI aliuliza: - Je, Serikali inachukua hatua gani kwa viongozi wanaowanyima wananchi kwa makusudi haki yao ya kuwa wanufaika wa TASAF?

Supplementary Question 2

MHE. MIRAJI J. MTATURU: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi.

Mheshimiwa Spika, zoezi la TASAF, kwa maana ya kukwamua familia maskini ni zoezi zuri. Huko nyuma lilikuwa liko kwenye package ya kuwalipa tu kwa ajili ya kuwasaidia kwenye mambo mbalimbali; sasa kumeongezwa package ya kuwapa hadhi halafu wanalipwa. Lakini maeneo mengi tumeanza kuona wazee wetu…

SPIKA: Swali lako Mheshimiwa Mtaturu.

MHE. MIRAJI J. MTATURU: Mheshimiwa Spika, tumekuwa wazee wetu wakitumikishwa wanafanya zaidi ya miaka 60 kitu ambacho sio kizuri katika maeneo yetu; je, Serikali inasemaje kuhusu jambo hili?

SPIKA: Ngoja kabla sijaiambia Serikali nataka nikuelewe wewe kwa hiyo ni jambo bayo kufanya kazi na kulipwa? Yaani uliza swali lako vizuri ili Serikali ijue inakujibuje, ni jambo bayo wale maskini kuambiwa wafanye kazi halafu walipwe?

MHE. MIRAJI J. MTATURU: Mheshimiwa Spika, si maskini watu wazee zaidi ya miaka 70 wanafanya kazi ya kuchimba mitaro, kutengeneza barabara, ambayo package hiyo ilikuwa inalenga kwa ajili ya vijana ambao wanatoka kwenye familia maskini swali langu ndio hilo.

Name

Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI
WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge Mtaturu kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba katika baadhi ya maeneo malalamiko haya yamekuwepo. Sisi kama Serikali tumekwishatoa mwongozo na huo ndio mwongozo unaoongoza shughuli za TASAF; kwamba wazee wote walio juu ya miaka 60 na akina mama wajawazito pamoja na watoto wadogo hawaruhusiwi kufanya kazi katika mazingira hayo ambayo yeye anayasema. Isipokuwa Serikali, na sheria vinaelekeza kwamba vijana wenye nguvu watafanya kazi kwa niaba ya wazee hao. Na kama itatokea kwamba mzee amelazimishwa basi sheria itafuata mkondo wake katika kuchukua hatua za msingi. (Makofi)

SPIKA: Sasa hayo maelezo ni ya jumla najaribu kuwaza mzee kama anao uwezo wa kufanya hiyo kazi halafu anyimwe; nadhani pengine huo mwongozo wa Serikali utazame. Kuna wazee kweli hawawezi kufanya kazi lakini wapo wazee wanaweza kufanya kazi na kama ameenda yeye kuomba hiyo kazi hoja ya kulazimisha ndiyo shida. Kama yeye ndio alienda kuomba kazi ni kwamba hiyo kazi angeweza kuifanya sehemu nyingine. Na hata humo ndani kuna wazee ambao wanaweza ubunge, wako wazee wanapewa mikataba hata Serikalini, sasa tukiweka kwa jumla namna hiyo Mheshimiwa Naibu Waziri hii inakaaje?

NAIBU WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS (MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA): Mheshimiwa Spika,
kwa niaba ya Serikali naomba nitoe maelezo mafupi juu ya jambo hili.

Mheshimiwa Spika, Mwongozo wa Serikali unataka wazee walio juu ya umri wa miaka 60 wasipewe kazi hizo kwa sababu ya ugumu wake; lakini inapotokea kwamba mazingira hayo yapo mwongozo unawaongoza kwamba wachukuliwe vijana ambao ndani ya kaya ile anayetoka huyo mzee ili wafanye kazi kwa niaba ya yule mzee. Sasa kumekuwa na incidence ambazo vijana wanakataa kwenda kufanya kazi au wakati mwingine wanawakatalia wazee wao kufanya kazi, kwa hiyo mzee kwa kutambua kwamba kuna hela ataikosa anaamua mwenyewe aende kufanya kazi hiyo. Sasa haya ni mazingira yaliyopo, lakini sisi kama Serikali tumeweka sheria na miongozo ambayo iko very strict, kwamba mzee aliyezidi miaka 60, mama mjamzito, mtoto chini ya miaka 18 hawaruhusiwi kufanya kazi.