Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Jafari Chege Wambura

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rorya

Primary Question

MHE. JAFARI W. CHEGE aliuliza: - Je, nini mpango wa Serikali kumaliza ujenzi wa zahanati kwa vijiji vilivyokamilisha ujenzi wa maboma?

Supplementary Question 1

MHE. JAFARI W. CHEGE: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri nataka kujua kwa kuwa kasi ya utoaji wa fedha hailingani na uhitaji wa maboma yanayohitajika kwa zahanati kwa vijiji vyote. Je, Serikali haioni sasa kuna umuhimu kwa mwaka huu wa bajeti kutenga fedha kukamilisha maboma yote ambayo yanahitajika kwenye vijiji vilivyohitaji ujenzi wa zahanati?

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili, kwa kuwa Serikali imekuwa ikitenga fedha shilingi milioni 500 mpaka shilingi milioni 700 kwa ajili ya ujenzi wa vituo vya afya kwenye kata 26 kwenye jimbo moja. Je, Serikali haioni sasa badala ya kupeleka fedha hizi kwenye umaliziaji wa kituo cha afya kimoja, fedha hii iende kukamilisha maboma yote yaliyojengwa na nguvu za wananchi kwenye eneo hilo hilo la jimbo ambao wanaweza wakakamilisha maboma 14 badala ya kituo cha afya kimoja kwenye eneo moja la wilaya moja?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Jafari Wambura Chege, Mbunge wa Jimbo la Rorya kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kasi ya ukamilishaji wa maboma ya zahanati nchini kote kwa kweli ni kubwa na Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameweka kipaumbele cha hali ya juu sana katika sekta ya afya na ndiyo maana katika kipindi cha miaka hii miwili zaidi ya maboma 1,600 ya zahanati yamekamilishwa na zahanati hizo zimeanza kutoa huduma. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kasi hii ya Serikali itaendelea ili kuhakikisha kwamba maboma hayo ambayo bado hayajakamilishwa yanakamilishwa na kuanza kutoa huduma kwa wananchi.

Mheshimiwa Spika, pili kuhusiana na kuacha kujenga vituo vya afya na kuweka kipaumbele kwenye zahanati, mfumo wa huduma za afya una utaratibu wa rufaa kwa ngazi. Ngazi za zahanati zina umuhimu wake katika ngazi ya vijiji lakini ngazi ya vituo vya afya ni rufaa ya zahanati na tunafahamu zahanati hazifanyi upasuaji na hazilazi kwa hiyo lazima tuendelee na nguvu za kujenga vituo vya afya sambamba na ujenzi wa zahanati.

Name

George Ranwell Mwenisongole

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbozi

Primary Question

MHE. JAFARI W. CHEGE aliuliza: - Je, nini mpango wa Serikali kumaliza ujenzi wa zahanati kwa vijiji vilivyokamilisha ujenzi wa maboma?

Supplementary Question 2

MHE. GEORGE R. MWENISONGOLE: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Nilitaka kujua ni vigezo vipi vinatumika katika kugawa hizo fedha za umaliziaji wa maboma ya zahanati kwani Jimbo la Mbozi tuna maboma zaidi ya 20 lakini kiasi kinachokuja ni kidogo?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa George Mwenisongole, Mbunge wa Jimbo la Mbozi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, vigezo ambavyo vinatumika kupeleka fedha ni idadi ya watu, umbali wa kijiji hicho kwenda kwenye kijiji chenye zahanati cha jirani zaidi. Lakini katika Jimbo la Mbozi pia Serikali imeendelea kupeleka fedha na nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge tutaendelea kupeleka fedha pia.

Name

Ndaisaba George Ruhoro

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngara

Primary Question

MHE. JAFARI W. CHEGE aliuliza: - Je, nini mpango wa Serikali kumaliza ujenzi wa zahanati kwa vijiji vilivyokamilisha ujenzi wa maboma?

Supplementary Question 3

MHE. GEORGE N. RUHORO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa fursa ya kuuliza swali la nyongeza. Jimbo la Ngara bado lina kata nyingi hazina vituo vya afya, je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha tunapata vituo vya afya kwenye kata hizo?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA- (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ndaisaba George, Mbunge wa Jimbo la Ngara kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali imeshafanya tathmini na kuainisha maeneo ya kimkakati ya kujenga vituo vya afya ikiwemo katika Kata za Jimbo la Ngara.

Name

Mohamed Lujuo Monni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chemba

Primary Question

MHE. JAFARI W. CHEGE aliuliza: - Je, nini mpango wa Serikali kumaliza ujenzi wa zahanati kwa vijiji vilivyokamilisha ujenzi wa maboma?

Supplementary Question 4

MHE. MOHAMED L. MONNI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, boma la zahanati ya Isusumya limekuwa la muda mrefu sana na tulileta maombi maalum. Nataka kujua sasa mpaka leo hatujajua nini kinaendelea, nini mpango wa Serikali wa kuhakikisha kwamba zahanati hiyo imekamilika?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mohamed Monni, Mbunge wa Jimbo la Chemba kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, nimuelekeze Mkurugenzi wa Halmashauri ya Chemba kutenga fedha za ukamilishaji wa Boma shilingi milioni 50 kwenye mwaka wa fedha ujao ili kukamilisha boma hili ambalo halmashauri imeona ni kipaumbele na tayari imeshaleta maombi maalum kwa ajili ya ukamilishaji.

Name

Ester Amos Bulaya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JAFARI W. CHEGE aliuliza: - Je, nini mpango wa Serikali kumaliza ujenzi wa zahanati kwa vijiji vilivyokamilisha ujenzi wa maboma?

Supplementary Question 5

MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza swali dogo la nyongeza. Serikali imekuwa ikitoa kiwango cha fedha kinachofanana katika umaliziaji wa maboma yote bila kuangalia hali halisi ya gharama za ujenzi.

Je, hamuoni kuna haja ya kufanya tathmini ili kutoa fedha kulingana na gharama ya ujenzi na maeneo husika ili maboma yaweze kukamilika kwa wakati?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ester Bulaya, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba tumekuwa tukitoa fedha kwa kiwango kinachofanana kwa maeneo tofauti na hivi sasa Serikali inafanya tathmini ya kutoa bei au BOQ kulingana na maeneo kijiografia, umbali lakini pia na gharama kutokana na maeneo hayo.

Name

Justin Lazaro Nyamoga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Primary Question

MHE. JAFARI W. CHEGE aliuliza: - Je, nini mpango wa Serikali kumaliza ujenzi wa zahanati kwa vijiji vilivyokamilisha ujenzi wa maboma?

Supplementary Question 6

MHE. JUSTIN L. NYAMOGA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, Kituo cha Afya cha Kata ya Ukumbi pamoja na Zahanati ya Kijiji cha Ilutila ni miaka 16 sasa ni maboma. Je, ni lini Serikali itamalizia kituo hicho cha afya pamoja na hiyo zahanati?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Justin Nyamoga, Mbunge wa Jimbo la Kilolo kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali ilishaweka utaratibu na tulishawaelekeza Wakurugenzi wa halmashauri kuleta vipaumbele vya maboma hasa ya vituo vya afya lakini pia na zahanati ambazo zinauhitaji mkubwa katika maeneo hayo. Kwa hiyo, nimwelekeze Mkurugenzi wa Halmashauri ya Kilolo kuwasilisha rasmi Ofisi ya Rais, TAMISEMI maombi ya vituo hivi ili Serikali iweze kuona namna ambavyo Serikali itatafuta fedha lakini pia na mapato ya ndani yatachangia kukamilisha vituo hivyo.

Name

Jackson Gedion Kiswaga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalenga

Primary Question

MHE. JAFARI W. CHEGE aliuliza: - Je, nini mpango wa Serikali kumaliza ujenzi wa zahanati kwa vijiji vilivyokamilisha ujenzi wa maboma?

Supplementary Question 7

MHE. JACKSON G. KISWAGA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kijiji cha Ndihuli kilichopo Kata ya Magulilwa kilijenga boma zaidi ya miaka saba. Je, ni lini sasa Serikali itatuonea huruma ipeleke fedha hapo tuweze kumalizia?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Jackson Kiswaga, Mbunge wa Jimbo la Kalenga kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, nimuombe Mheshimiwa Mbunge awasilishe maombi hayo kupitia kwa Mkurugenzi ili tuweze kuona namna ambavyo tutatenga fedha kwenye bajeti za miaka ijayo kwa ajili ya kukamilisha boma hili kwa ajili ya zahanati.

Name

Daimu Iddi Mpakate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kusini

Primary Question

MHE. JAFARI W. CHEGE aliuliza: - Je, nini mpango wa Serikali kumaliza ujenzi wa zahanati kwa vijiji vilivyokamilisha ujenzi wa maboma?

Supplementary Question 8

MHE. DAIMU I. MPAKATE: Mheshimiwa Spika, ahsante, Jimbo la Tunduru Kusini lina maboma saba yako katika hatua mbalimbali katika Vijiji vya Mkapunda, Chuwala, Ukandu, Nazya pamoja na Lupanji; je, Serikali ina mpango gani sasa wa kupeleka fedha kumalizia maboma hayo ya zahanati?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Iddi Mpakate, Mbunge wa Jimbo la Tunduru Kusini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, tumekwisha elekeza na nirudie kuwakumbusha Wakurugenzi wa halmashauri kuhakikisha wanaweka vipaumbele vya ujenzi na ukamilishaji wa maboma ya zahanati katika maeneo yenye uhitaji mkubwa. Kwa hiyo, maboma haya saba ambayo Mheshimiwa Mbunge ameyataja, Ofisi ya Rais TAMISEMI tutachukua lakini tutafanya mawasiliano na Wakurugenzi ili tuone yapi tuanze nayo kwa awamu lakini tutaendelea kutenga fedha kwa kadiri ya upatikanaji wa fedha.

Name

Deo Kasenyenda Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makambako

Primary Question

MHE. JAFARI W. CHEGE aliuliza: - Je, nini mpango wa Serikali kumaliza ujenzi wa zahanati kwa vijiji vilivyokamilisha ujenzi wa maboma?

Supplementary Question 9

MHE. DEO K. SANGA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Kuna boma la Mji mwema, Mkalanga pamoja na Kata ya Kivavi, ni lini Serikali itamalizia maboma ambayo wananchi wameshayajenga?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Deo Kasenyenda Sanga, Mbunge wa Jimbo la Makambako kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, boma hili la Mji mwema lakini na Mkalanga ni maboma ambayo tayari tulishayaingiza kwenye bajeti ya mwaka ujao wa fedha. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tutakwenda kutekeleza ukamilishaji wa maboma hayo mwaka ujao wa fedha.

Name

Furaha Ntengo Matondo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JAFARI W. CHEGE aliuliza: - Je, nini mpango wa Serikali kumaliza ujenzi wa zahanati kwa vijiji vilivyokamilisha ujenzi wa maboma?

Supplementary Question 10

MHE. FURAHA N. MATONDO: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa kunipa nafasi. Wananchi wa Kata ya Nyasaka Mtaa wa Kiloleli B wamenunua kiwanja kwa ajili ya kujenga zahanati. Je, ni lini Serikali itawajengea zahanati katika kiwanja hicho?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Furaha, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, niwapongeze Kijiji hiki kwa kununua eneo kwa ajili ya ujenzi wa zahanati lakini nimwelekeze Mkurugenzi kuanza kutenga fedha kwa awamu kwa ajili ya ujenzi wa zahanati hii.