Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 2 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 16 2023-04-05

Name

Jafari Chege Wambura

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rorya

Primary Question

MHE. JAFARI W. CHEGE aliuliza: -

Je, nini mpango wa Serikali kumaliza ujenzi wa zahanati kwa vijiji vilivyokamilisha ujenzi wa maboma?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba wa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Jafari Wambura Chege, Mbunge wa Rorya kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali imeendelea kutoa fedha kwa ajili ya ukamilishaji wa maboma ya zahanati yaliyojengwa kwa nguvu za wananchi ambapo katika kipindi cha mwaka wa fedha wa 2017/2018 hadi 2021/2022 kiasi cha shilingi bilioni 71.95 zimetolewa kwa ajili ya ukamilishaji wa maboma 1,214 ya zahanati nchini kote. Aidha, katika mwaka wa fedha 2022/2023 Serikali imetenga kiasi cha shilingi bilioni 15 kwa ajili ya ukamilishaji wa maboma ya zahanati 300, hadi kufikia Februari, 2023 kiasi cha shilingi bilioni 14.6 zimekwishatolewa.

Mheshimiwa Spika, Jumla ya zahanati 762 kati ya 1,514 ujenzi umekamilika na zimeanza kutoa huduma. Aidha, Ujenzi wa maboma 752 ya zahanati upo katika hatua mbalimbali za ukamilishaji.

Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea kutenga bajeti kwa ajili ya ukamilishaji wa maboma ya zahanati yaliyojengwa kwa nguvu za wananchi.