Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Agnes Mathew Marwa

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AGNES M. MARWA aliuliza: - Je, ni vikundi vingapi vya wanawake na vijana vimewezeshwa kufanya uvuvi wa vizimba Ziwa Victoria?

Supplementary Question 1

MHE. AGNES M. MARWA: Mheshimiwa Spika, je, ipo ruzuku ama mikopo nafuu ya kuwezesha miradi hii ya vizimba ili kufanya uvuvi kuwa wa kisasa zaidi?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, je, Wizara ina mpango gani wa kuendelea kutoa elimu kuwawezesha wavuvi au wananchi wanaozunguka Ziwa Victoria kuwa na uelewa zaidi na haswa Mkoa wa Mara ambao bado hawajapata elimu hiyo? (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu maswali madogo mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Agnes Mathew Marwa, Mbunge wa Viti Maalum kutoka Mkoa wa Mara, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, natambua kwamba Mheshimiwa Mbunge ni mvuvi na ni Mchuuzi na ni mtu ambae anaipenda sana hiyo kada. Nimhakikishie tu kwamba Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi tunazo fedha ambazo ni za masharti nafuu kwa ajili ya wafugaji wa samaki kwa vizimba kwa vijana. Eneo la pili ni kwamba mpango wa kutoa elimu upo na sasa hivi tumeanza na programu za vijana atamizi ambao wanakuwa wakifundishwa juu ya ufugaji wa samaki na elimu ya viumbe maji katika maeneo ambayo yanazungukwa na bahari, maziwa ambapo vijana wengi wanahusika na kazi hiyo.

Mheshimiwa Spika, hivyo nimhakikishie tu Mheshimiwa Agnes Marwa kwamba kazi hiyo itafanyika. Ahsante sana.

Name

Stella Ikupa Alex

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AGNES M. MARWA aliuliza: - Je, ni vikundi vingapi vya wanawake na vijana vimewezeshwa kufanya uvuvi wa vizimba Ziwa Victoria?

Supplementary Question 2

MHE. STELLA I. ALEX: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa fursa; nini mkakati wa Serikali kutoa kipaumbele kwa vijana wenye ulemavu wenye sifa kwenye mradi huu wa uvuvi wa vizimba? Ahsante.

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Stella Ikupa kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali ina mpango na katika mipango yetu tumewapa vipaumbele watu wote wenye ulemavu na katika elimu ambayo tunaitoa sasa hivi moja wapo ya kigezo ni kuwa na wavuvi ambao wanatokana na watu wenye mahitaji maalum, ahsante sana. (Makofi)