Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 1 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Waziri wa Mifugo na Uvuvi 15 2023-04-04

Name

Agnes Mathew Marwa

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AGNES M. MARWA aliuliza: -

Je, ni vikundi vingapi vya wanawake na vijana vimewezeshwa kufanya uvuvi wa vizimba Ziwa Victoria?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante sana na kabla sijajibu swali, naomba kwa kifupi sana nimshukuru Mheshimiwa Rais kwa kuendelea kuniamini na kuniteua kuwa Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi. Nimhakikishie tu Mheshimiwa Rais ameweka mtu sahihi, mahali sahihi na kazi itafanyika. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mifugo na Uvuvi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Agnes Mathew Marwa, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2021/2022, Wizara ya Mifugo na Uvuvi kupitia Wakala ya Elimu na Mafunzo ya Uvuvi (FETA) Nyegezi Mwanza ilitoa mafunzo ya ufugaji samaki kwa vizimba kwa vijana 288 (wanaume 208 na wanawake 80). Vijana hao walitoka katika Wilaya za Nyamagana – 74; Ilemela – 54; Magu – 31; Misungwi – 21; Ukewere – 51; Sengerema - 28 na Buchosa - 29.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2022/2023, Serikali imetenga shilingi bilioni 20 kwa ajili ya kuwawezesha wakuzaji viumbe maji nchini. Kati ya fedha hizo shilingi bilioni 15.1 zitatolewa kwa wafugaji samaki kwa vizimba katika Ziwa Victoria kama mikopo ya pembejeo kwa masharti nafuu kupitia Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB). Jumla ya wananchi 3,154 wanatarajiwa kunufaika kwa kupata mikopo ya vizimba, vifaranga na chakula cha samaki. Kati ya hao vijana ni 241, wanawake 290 na kampuni mbili za wanawake. Ahsante sana.