Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Kiswaga Boniventura Destery

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Magu

Primary Question

MHE. BONIVENTURA D. KISWAGA aliuliza:- Zahanati za Nyang‟hanga, Salongwe, Nsola, Bundilya, Nyamahanga, Nyashingwe, Chabula, Ikengele, Isangijo, Langi na Lutale ziko kwenye hatua za ukamilishaji. Je, ni lini Serikali itazikamilisha zahanati hizo?

Supplementary Question 1

MHE. BONIVENTURA D. KISWAGA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali na nazidi kumpongeza Mheshimiwa Naibu Waziri kwa kadri anavyochapa kazi kuhakikisha kwamba anatoa majibu yanayoridhisha.
Mheshimiwa Naibu Spika, wa kuwa zahanati hizi wananchi walizijenga, Nyang‟hanga, Salongwe, Bundilya, Nsola, Nyamahanga, Nyashigwe, Chabula, Ikengele, Isangijo, Langi na Lutale; na ziko hatua za kukamilisha ili waweze kupata huduma; na kwa kuwa bajeti ya mwaka 2015/2016 inaelekea mwisho; je, Serikali inaweza kutupatia fedha hizi kwa haraka ili tuweze kukamilisha miradi hii na wanachi wapate huduma?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa Ilani yetu ya Chama cha Mapinduzi inasema kila kijiji kiwe na zahanati, na wananchi wetu wamekuwa wakiwahi kutimiza wajibu wao kwa maana ya kujenga maboma haya.
Je, Serikali ina mpango gani wa kuharakisha utekelezaji wa ilani hii ili wananchi waweze kupata huduma hiyo?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuweka kumbukumbu sawa, miongoni mwa maswali mengi niliyoyapata yalikuwa ni maswali kutoka Jimbo la Magu na miongoni mwa ziara yangu ya kwanza katika nafasi yangu Mheshimiwa Rais aliyonipa nilianza Jimbo la Magu kwa Mheshimiwa Kiswaga. Kwa hiyo. nimpongeze sana kwa kazi kubwa anayofanya na katika ziara hiyo niliona miradi mbalimbali ukiwemo mradi wa ujenzi huu wa zahanati. Naomba nikiri wazi, ni kweli fedha hazijaenda. Lakini Serikali kama tulivyosema, kwamba tumejipanga.
Mheshimiwa Naibu Spika, watu wate mnafahamu kwamba mara baada ya uchaguzi miradi mingi ilikuwa imesimama, lakini mchakato mkubwa uliofanyika kuanzia mwezi Januari mpaka tunapozungumza hivi, angalau fedha nyingi zimeenda katika miradi mbalimbali. Wakati napita kwa Mheshimiwa Kiswaga miradi mingi ilikuwa imesimama. Katika kipindi hichi Jimbo la Magu limepatiwa karibuni shilingi bilioni 4.9 baada ya msukumo mkubwa wa Serikali katika miradi mingine ya maendeleo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo najua Serikali itaendelea ku-push kuhakikisha kwamba mambo yanakwenda. Najua katika zahanati fedha hazijaenda, lakini hata zile fedha za maji mlizokuwa mmeomba Serikali imeweza kuzipeleka kule. Hii inamaana kwamba Serikali inawajali watu wa Magu. Kwa hiyo nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali itaendelea kufanya juhudi zilezile.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika suala zima la mpango mpana wa jinsi gani maboma haya yatamaliziwa nimesema hapa mara kadhaa. Ni kwamba ni kweli jukumu letu ni kumalizia maboma. Lakini katika ajenda ya sera ya Serikali na Ilani ya Uchaguzi wa Chama cha Mapinduzi tumejielekeza kwenye vituo vya afya katika kila kata na zahanati katika kila kijiji.
Mheshimiwa Naibu Spika, ndiyo maana Waziri wangu mwenye dhamna hapa hata jana alisema mpango wetu mpana sasa hivi ni kuhakikisha angalau kila mwaka katika Halmashauri zote tujenge kituo kimoja cha afya, lakini halikadhalika ujenzi wa zahanati na kumalizia yale maboma. Imani yangu kubwa ni kwamba kwa sababu tuna Halmashauri 181 tukijenga kituo kimoja cha afya, maana yake tulikuwa tumejenga kwa mwaka mmoja vituo vya afya 181, ni mapinduzi makubwa kwa mwaka mmoja peke yake.
Mheshimiwa Naibu Spika, imani yangu ndani ya miaka mitano tutafanya mabadiliko makubwa, na mwisho wa siku ni kwamba Sera na Ilani ya Chama cha Mapinduzi itatekelezeka kwa mipango hii tunaifanya pamoja baina ya TAMISEMI, Wizara ya Afya na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Kamati ya Bajeti.

Name

Augustino Manyanda Masele

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbogwe

Primary Question

MHE. BONIVENTURA D. KISWAGA aliuliza:- Zahanati za Nyang‟hanga, Salongwe, Nsola, Bundilya, Nyamahanga, Nyashingwe, Chabula, Ikengele, Isangijo, Langi na Lutale ziko kwenye hatua za ukamilishaji. Je, ni lini Serikali itazikamilisha zahanati hizo?

Supplementary Question 2

MHE. AUGUSTINO M. MASELE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ili niweze na mimi kuuliza swali moja dogo la nyongeza.
Mheshimwia Naibu Spika, kwa kuwa changamoto zinazowakabili wananchi wa Jimbo la Magu zinafanana sana na changamoto zinazolikabili Jimbo la Mbogwe, ambapo wananchi katika Kata za Ikunguigazi, Lolangulu, Ikobe na Bukwande wamejenga majengo yao ya maboma kwa ajili ya vituo vya afya lakini nguvu zao zikawa zimepelea. Je, Serikali iko tayari sasa kuwaunga mkono ili kuweza kukamlisha vituo hivyo vya afya?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kumjibu Mheshimiwa Augustino Manyanda Masele mjukuu wa Mzee Ulega kuwa tumeliongelea suala la zahanati na tukiwa pale Geita wakati Mheshimiwa Mama Suluhu Hassan alipokuwa akizindua hospitali kubwa ya Geita. Nimesema hapa katika majibu yangu ya msingi, kwamba mambo makubwa tunaenda kuyafanya. Sasa hivi tunafanya tathimini ili tuangalie jinsi ya gani ya kufanya.
Kwa hiyo nikuhakikishie Mheshimiwa Augustino kwamba tutakupa kipaumbele kikubwa zaidi na kwa sababu katika ratiba ambayo nimeitengeneza leo, katika ziara yangu miongoni mwa maeneo nitakayopita Jimbo lako nimeliweka kutokana na kunisukumasukuma sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, nadhani tukifika kule tunaweza kuangali hata structure ya majengo yenyewe na kukupa kipaumbe ili wanchi wako wa Jimbo la Mbogwe kupata huduma ya afya.

Name

Richard Mganga Ndassa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sumve

Primary Question

MHE. BONIVENTURA D. KISWAGA aliuliza:- Zahanati za Nyang‟hanga, Salongwe, Nsola, Bundilya, Nyamahanga, Nyashingwe, Chabula, Ikengele, Isangijo, Langi na Lutale ziko kwenye hatua za ukamilishaji. Je, ni lini Serikali itazikamilisha zahanati hizo?

Supplementary Question 3

MHE. RICHARD M. NDASSA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Naomba nimuulize Mheshimiwa Waziri, kwa sababu kazi ya ujenzi wa zahanati ni kazi nyingine, ujenzi wa vituo vya afya ni kazi nyingine, upelekaji wa tiba ni kazi nyingine. Je, Serikali kwa sababu inajua kwamba upo upungufu mkubwa sana wa wataalam katika ngazi zote, imejipanga namna gani kuhakikisha kwamba zahanati na vituo vyote vile vinakuwa na waganga wa kutosha?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, juu ya mpango wa Serikali tumezungumza hapa. Ni kweli tunajenga structures hizi lakini lazima tupeleke vifaa tiba, dawa na wataalam. Hili tumelizungumza na mlikuwa mnajua tulikuwa na mchakato katika suala zima la ajira, lakini kutokana na changamoto ya watumishi hewa, maelekezo yametoka ya kumaliza kufanya analysis ya kuangalia watumishi hewa na baadaye tutaendelea na mchakato wa kupata ajira mpya na vijana wetu watapata kazi katika maeneo ya site.
Mheshimiwa Naibu Spika, ninamuomba Mheshimiwa Ndassa, tuwe na subira, jambo hili linakwenda vizuri, kwa sababu vijana wanaopakuliwa kutoka vyuoni, utaratibu wa Serikali utakapokaa vizuri sasa watapelekwa maeneo husika baada ya kupata ajira ili wakawapatie wananchi huduma ya afya.

Name

Dr. Dalaly Peter Kafumu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igunga

Primary Question

MHE. BONIVENTURA D. KISWAGA aliuliza:- Zahanati za Nyang‟hanga, Salongwe, Nsola, Bundilya, Nyamahanga, Nyashingwe, Chabula, Ikengele, Isangijo, Langi na Lutale ziko kwenye hatua za ukamilishaji. Je, ni lini Serikali itazikamilisha zahanati hizo?

Supplementary Question 4

MHE. DKT. DALALY P. KAFUMU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kama ilivyo katika swali la msingi, Wilaya ya Igunga nayo ina zahanati kama Jogohya, Mbutu, Mwazizi na Kalangale ambazo hazijakamilishwa. Je, Serikali nayo itaelekeza jicho lake huko kwenye Wilaya ya Igunga pia?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Dalaly Peter Kafumu kwamba eneo lako pale, mpaka Jimbo la Manonga kwa Mheshimiwa Gulamali kuwa ni miongoni mwa eneo ambayo nimepanga kuyatembelea. Kwa sababu licha ya suala zima la umaliziaji wa zile zahanati, lakini pia kuna vituo vya afya ambavyo vimejengwa ambavyo hata upatikanaji wa vifaa vyake inaonekana kuna uchakachuaji umefanyika. Na ndio maana nimepanga ziara maalum kwa Wilaya yako ya Igunga licha ya kuangalia namna ya kumaliza zile structure, lakini pia kuangalia juu ya habari niliyoipata ya ubadhirifu uliofanyika katika baadhi ya maeneo. Kwa hiyo lazima nifike site kuja kupambana na hayo yaliyotokea.
Mheshimiwa Naibu Spika, na naomba nikuhakikishie kwamba wale wote ambao inaonekana wamefanya ubadhirifu katika majengo ya afya tutawachukulia hatua. Uwe na amani ya kutosha, Serikali iko kwa ajili ya kupambana na mambo ya maendeleo katika nchi yetu.