Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 47 Health and Social Welfare Ofisi ya Rais TAMISEMI. 401 2016-06-21

Name

Kiswaga Boniventura Destery

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Magu

Primary Question

MHE. BONIVENTURA D. KISWAGA aliuliza:-
Zahanati za Nyang‟hanga, Salongwe, Nsola, Bundilya, Nyamahanga, Nyashingwe, Chabula, Ikengele, Isangijo, Langi na Lutale ziko kwenye hatua za ukamilishaji.
Je, ni lini Serikali itazikamilisha zahanati hizo?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Boniventura Destery Kiswaga Mbunge wa Magu kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, katika bajeti ya mwaka wa fedha 2015/2016 Halmashauri ya Wilaya ya Magu imetengewa shilingi milioni 160 kwa ajili ya ukamilishaji wa ujenzi wa zahanati kumi na tano ambazo ziko katika hatua mbalimbali. Vilevile katika mwaka 2016/2017 zimetengwa shilingi milioni 212.7 kwa ajili ya ukamilishaji wa zahanati hizo.
Mheshimiwa Naibu Spika, azma ya Serikali ni kuhakikisha tunakamilisha majengo hayo ili huduma zianze kutolewa. Kama nilivyoeleza hapa Bungeni mara kadhaa, hivi sasa tunakamilisha tathmini ya ujenzi wa miundombinu ya zahanati na vituo vya afya ili kuandaa mpango wa haraka utakaosaidia kukamilisha ujenzi wa majengo hayo muhimu kwa nchi nzima.