Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Muharami Shabani Mkenge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bagamoyo

Primary Question

MHE. MUHARAMI S. MKENGE aliuliza: - Je, kwa mwaka 2020/2021 na 2021/2022 ni kiasi gani cha gawio kimetolewa na eneo la Utalii Kaole kwa Halmashauri ya Bagamoyo?

Supplementary Question 1

MHE. MUHARAMI S. MKENGE: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, lakini nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; je Serikali haioni iko haja sasa ya kuondoa hizo sheria, miongozo na kanuni ili wananchi wa Kaole waweze kupatiwa gawio kwa kile ambacho kipo katika mji wao?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; je ni lini Serikali sasa ina mpango wa kuwatumia wazee wa Kaole kuelezea historia ya magofu ya kale pamoja na kaole kwa wageni wanaokuja badala ya kuwatumia waajiriwa ambao historia hiyo wameisoma kwenye vitabu?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, ahsante na naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mharami Shabani, Mbunge wa Bagamoyo kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwa namna ambavyo sasa hivi Wizara ya Maliasili na Utalii makusanyo yake yanaenda Mfuko Mkuu hatuoni haja ya kurekebisha sheria hii kwa sababu makusanyo yote yanayokusanywa yanaenda Mfuko Mkuu na yanapofika kwenye Mfuko Mkuu, halmashauri zinapokea ruzuku mbalimbali ambazo zinatoka katika Mfuko Mkuu. Kwa hiyo fedha yote inayokusanywa katika maeneo haya tuna uhakika kwamba inaenda kulenga wananchi wa Tanzania nzima kutokana na masuala mazima ya utalii.

Mheshimiwa Spika, hili lingine alilosema la kutumia wazee tunalipokea, tutawashirikisha wazee wa Bagamoyo pamoja na maeneo mengine zilipo malikale ili tuweze kuipata historia kamili ya Tanzania pamoja na wazee wetu waliotutangulia, ahsante.