Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 1 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 14 2023-04-04

Name

Muharami Shabani Mkenge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bagamoyo

Primary Question

MHE. MUHARAMI S. MKENGE aliuliza: -

Je, kwa mwaka 2020/2021 na 2021/2022 ni kiasi gani cha gawio kimetolewa na eneo la Utalii Kaole kwa Halmashauri ya Bagamoyo?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Muharami Shabani Mkenge, Mbunge wa Jimbo la Bagamoyo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Kituo cha Magofu ya Kaole kilianza kutambuliwa na kuhifadhiwa kisheria mwaka 1937 ilipoanzishwa Sheria ya Uhifadhi wa Majengo ya Kihistoria, kipindi cha utawala wa Mwingereza na kwa sasa yanalindwa kwa Sheria ya Mambo ya Kale, Sura 333. Hapo awali vituo vya mambo ya kale vilitumika zaidi katika masuala ya tafiti na elimu hivyo kutembelewa zaidi na wanafunzi wa shule za msingi, sekondari na vyuo.

Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa Sheria, Kanuni na miongozo iliyopo hakuna gawio lolote linalotolewa kwa Halmashauri kutokana na mapato ya vituo vya malikale. Aidha, Magofu ya Kaole yanatoa fursa kwa wananchi wa Halmashauri ya Bagamoyo kunufaika kiutalii kwa kuuza bidhaa mbalimbali kwa watalii kama vile vitu vya kiutamaduni, vyakula na kutoa huduma ya malazi. Kwa kufanya hivyo, halmashauri hunufaika kupitia tozo mbalimbali kwa wafanyabiashara hao.