Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Jacquline Andrew Kainja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JACQUELINE K. ANDREW aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kutenga bajeti kwa Hifadhi changa za utalii ili kukuza utalii katika hifadhi hizo?

Supplementary Question 1

MHE. JACQUELINE K. ANDREW: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri ya Serikali, nina maswali mawili. Swali langu la kwanza; katika mikoa yetu ambayo ina hifadhi changa, Wakuu wetu wa Mikoa wamejitahidi kujitokeza

kuhakikisha wanatangaza utalii katika hifadhi hizi changa. Je, Serikali ina mpango gani katika kuhakikisha inasaidia viongozi hawa wa mikoa ili kuweza kukuza utalii katika hizi hifadhi changa na tukizingatia bado miundombinu ni mibovu, magari pia hayatoshi, wanapata wakati mgumu hasa wanapokuwa wanafanya kazi za kutangaza hifadhi hizi kujikuta sasa inabidi waazime magari kutoka sehemu zingine, tunaonaje kama Serikali tuweze kusaidia kutangaza sekta hii ya Maliasili na Utalii?

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili; bado tunachangamoto nyingi kwenye upande wa ajira. Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha ajira zinapatikana na kukuza sekta hii ya utalii hasa katika hifadhi hizi changa, ahsante.

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Jacquiline Kainja, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba Serikali kwa sasa imejikita katika maeneo mapya ya utalii zikiwemo hifadhi hizi ambazo imezitaja na malengo makuu ni kuhakikisha kwamba tunapanua wigo wa namna ambavyo watalii wataweza kufika katika maeneo hayo. Mikoa yote ya Tanzania tumeendelea kuwahimiza waendelee kuhamasisha utalii ikiwemo utalii wa ndani lakini pia tumejikita kuboresha miundombinu zikiwemo barabara, maeneo ya malazi na chakula ili sasa iwe rahisi kwa watalii kuweza kufika katika maeneo hayo. Kwa hiyo tunaendelea kuwahimiza Wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya waendelee kuhamasisha masuala mazima ya utalii.

Mheshimiwa Spika, suala lingine ameongelea kuhusu ajira. Tumeendelea kuwasiliana na Ofisi ya Rais, Menejimenti Utumishi na Utawala Bora kuangalia namna ya kuongeza watumishi ambao tutawasambaza katika maeneo mapya yaliyoko katika hifadhi hizo.