Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 1 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 13 2023-04-04

Name

Jacquline Andrew Kainja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JACQUELINE K. ANDREW aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kutenga bajeti kwa Hifadhi changa za utalii ili kukuza utalii katika hifadhi hizo?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante na kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Jacqueline Kainja Andrew, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia fedha za Mpango wa Maendeleo na Mapambano dhidi ya UVIKO-19, tayari ilishaanza mchakato wa kuboresha hifadhi changa 17 za utalii ikiwemo kuboresha miundombinu ya barabara, huduma za malazi na chakula na maeneo ya uwekezaji ambapo tayari wawekezaji wameonesha nia ya kuwekeza. Hifadhi za Taifa changa zilizopo katika mkakati huo ni Burigi-Chato, Gombe, Ibanda-Kyerwa, Katavi, Kigosi, Kisiwa cha Rubondo, Kisiwa cha Saanane, Kitulo, Milima ya Mahale, Milima ya Udzungwa, Mikumi, Mkomazi, Mto Ugalla, Nyerere, Ruaha, Rumanyika-Karagwe na Saadani.

Mheshimiwa Spika, Serikali pia imeendelea kutenga fedha kwa ajili ya kuboresha hifadhi hizo kwa lengo la kukuza utalii na kuongeza mapato. Maboresho hayo yanaenda sambamba na utekelezaji wa Programu ya Tanzania, the Royal Tour ambapo kwa sasa Serikali imejikita zaidi kwenye maeneo mapya ya utalii zikiwemo hifadhi hizo.