Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Stella Simon Fiyao

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. STELLA S. FIYAO aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Bandari kavu katika Mji wa Tunduma?

Supplementary Question 1

MHE. STELLA S. FIYAO: Mheshimiwa Spika, nashukuru. Pamoja na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri naomba kuwa na maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; kwa kuwa Serikali imetambua uwepo na umuhimu wa Bandari Kavu ndani ya Mji wa Tunduma na tayari Halmashauri ya Mji wa Tunduma imetenga zaidi ya ekari 2,000 kwa ajili ya uwekezaji wa bandari kavu. Sasa nataka kujua je, ni sekta ngapi binafsi ambazo zimefikiwa mpaka sasa ili kuja kuwekeza bandari kavu ndani ya Mji wa Tunduma?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; kwa kuwa Taifa sasa lipo katika ushindani wa kibiashara; je hatuoni kuchelewachelewa tunaweza tukaleta matokeo hasi? Ahsante sana.

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI UCHUKUZI (MHE. FREDY A. MWAKIBETE): Mheshimiwa Spika, ahsante, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Stella Simon Fiyao, Mbunge wa Viti Maalumu kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli Halmashauri ya Tunduma ina eneo la kuweza kujenga bandari hii kavu na sekta ambazo ziko tayari kwa ajili ya uwekezaji katika eneo hili la bandari kavu, kuna Sekta ya Kilimo, Sekta ya Viwanda na Sekta ya Mifugo.

Mheshimiwa Spika, kwa upande wa swali lake la pili, suala la kuchelewachelewa. Kimsingi Serikali imechukua hatua za kuongea na watu binafsi na ndio maana hadi sasa tupo kwenye majadiliano ya mwisho ili eneo la Mpemba ambalo litakuwa linaunganisha upande wa Malawi pamoja na Zambia na DRC liweze kujengwa Bandari hii kavu, ahsante.

Name

Abdulaziz Mohamed Abood

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Mjini

Primary Question

MHE. STELLA S. FIYAO aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Bandari kavu katika Mji wa Tunduma?

Supplementary Question 2

MHE. ABDUL-AZIZ M. ABOOD: Mheshimiwa Spika, Morogoro ina barabara mbili kuu zinazounganisha nchi za SADC na Afrika Mashariki. Morogoro ilitenga hekari 500 kwa ajili ya bandari kavu, je Serikali ina mpango gani wa kujenga Bandari Kavu katika Mji wa Morogoro?

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI UCHUKUZI (MHE. FREDY A. MWAKIBETE): Mheshimiwa Spika, ahsante, napenda kujibu swali moja la nyongeza la Mheshimiwa Abdul-Aziz, Mbunge wa Morogoro kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli Morogoro pia tuna eneo kwa ajili ya ujenzi wa Bandari Kavu na kwa kuwa reli yetu SGR itaanza kazi hivi karibuni na katika mwaka wa fedha ujao nimwombe Mheshimiwa Mbunge apitishe bajeti yetu ya Wizara ya Ujenzi kwa kuwa ni miongoni mwa Bandari Kavu zitakazojengwa katika mwaka wa 2023/2024. Ahsante.