Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 1 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 10 2023-04-04

Name

Stella Simon Fiyao

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. STELLA S. FIYAO aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Bandari kavu katika Mji wa Tunduma?

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. FREDY A. MWAKIBETE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Stella Simon Fiyao, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) imekamilisha zoezi la kufanya upembuzi yakinifu wa kuendeleza bandari kavu zote nchini ikiwemo ya Bandari Kavu ya Tunduma.

Mheshimiwa Spika, Kiuchumi na kibiashara, Bandari Kavu ya Tunduma ni muhimu sana kwa sababu ndilo langu kuu la kupitisha bidhaa za nchi za Zambia, DRC na nchi nyingine kusini mwa Afrika.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa Bandari hiyo ina mvuto zaidi wa kibishara, mpango wa Serikali ni kushirikisha sekta binafsi ikiwa pamoja na halmashauri kwenye maeneo husika. TPA inaendelea na vikao vya wadau ili kushawishi uwekezaji huo.