Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza: - Je, ni lini barabara ya Haydom kwenda Mogitu - Katesh itajengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 1

MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Kwa kuwa barabara hii ina vipande vingi; je, kipande hiki cha Labay kwenda Hydom na cha Dongobesh kwenda Dareda mnakijenga lini?
Mheshimiwa Spika, swali la pili, kwa kuwa kipande hiki cha Mbulu kuja Garbabi mmeshamuweka mkandarasi pale na yuko site na hamjamlipa advance payment na hajengi tena barabara;

Je, ni lini mnamlipa advance payment ili ajenge barabara au mpaka turuke tena?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Flatei Gregory Massay, Mbunge wa Mbulu Vijijini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kipande cha Mbulu- Garbabi mkandarasi yuko site, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba hajatoka site yupo; na mudo siyo mrefu fedha aliyokuwa anaidai, kwa sababu ilikuwa ni sanifu na jenga, italipwa muda siyo mrefu na kwa hiyo tunaamini kwamba kasi itazidi.
Mheshimiwa Spika, barabara ya Dareda – Dongobesh ipo kwenye hatua za manunuzi na sasa tuko kwenye hatua ya majadiliano na mkandarasi. Ahsante

WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Spika, nimpongeze Mheshimiwa Naibu Waziri, kwa majibu mazuri. Nilitaka kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge na wala asiruke sarakasi tena, fedha ile Wizara ya Ujenzi walishaleta maombi yale na tunakamilisha maandalizi tutatoa ile fedha ili mkandarasi asikwame. Na tumeongea na wenzetu wa Wizara ya Ujenzi tutapata majumuisho hata maeneo mengine ambayo yalikuwa na uhitaji wa aina hiyo ili tuweze kukamilisha na kazi zisikwame.

Name

Leah Jeremiah Komanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Meatu

Primary Question

MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza: - Je, ni lini barabara ya Haydom kwenda Mogitu - Katesh itajengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 2

MHE. LEAH J. KOMANYA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru; je, ni lini Serikali itajenga kwa kiwango cha lami kilometa 25 katika maingilio ya Daraja la Sibiti ili kunusuru mmomonyoko kwa kuwa barabara iko juu ya mbuga?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Leah Komanya, Mbunge wa Meatu kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli Daraja la Sibiti linatakiwa kujengwa approach roads, yaani barabara za maingilio kilometa 25. Taratibu za kumpata mkandarasi ambaye atajenga zinaendelea. Hata hivyo bado katika hii barabara ndiyo barabara ambayo mpango wa EPC+F barabara ndefu pia itapita hapo. Ahsante.

Name

Maimuna Ahmad Pathan

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza: - Je, ni lini barabara ya Haydom kwenda Mogitu - Katesh itajengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 3

MHE. MAIMUNA A. PATHAN: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Je, ni lini barabara ya kutoka Masasi kwenda Liwale kupitia Nachingwea itajengwa kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara ya Masasi – Nachingwea – Liwale ni kati ya barabara saba ambazo zilichaguliwa kuingia kwenye mpango wa EPC+F; na tunavyoongea sasa hivi upande wa ufundi zimeshakamilishwa ziko kwenye upande wa fedha sasa ya kufanyiwa tathmini.

Name

Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Primary Question

MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza: - Je, ni lini barabara ya Haydom kwenda Mogitu - Katesh itajengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 4

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Spika, ahsante sana.

Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Karatu – Mbulu kilometa 76 kama ilivyowekwa kwenye bajeti ya mwaka huu?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Zacharia Issaay, Mbunge wa Mbulu Vijijini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara ya Karatu – Mbulu – Haydom – Sibiti ndiyo barabara ambazo kati ya zile barabara saba ipo kwenye mpango huu wa EPC+F. Kwa hiyo, kama itakavyokuwa imekamilika basi kilometa hizo 76 itakuwa ni sehemu ya ujenzi wa hiyo barabara.

Name

Catherine Valentine Magige

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza: - Je, ni lini barabara ya Haydom kwenda Mogitu - Katesh itajengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 5

MHE. CATHERINE V. MAGIGE: Mheshimiwa Spika, wananchi wa Monduli wamekuwa wakipata changamoto kubwa ya barabara inayotokea Monduli Chini kwenda Monduli Juu nyumbani kwa Sokoine.

Je, Serikali haioni umuhimu wa kujenga barabara hii katika kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Catherine Magige, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara zote ambazo ni za mkoa zinatakiwa zijengwe kwa kiwango cha lami, lakini kinacho gomba hapa ni bajeti kwa hiyo tunakwenda kwa awamu.

Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba barabara hii kwa umuhimu wake pia ipo kwenye mpango lakini itaanza kujengwa pale ambapo bajeti itaruhusu. Ahsante.

Name

Shabani Hamisi Taletale

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini Mashariki

Primary Question

MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza: - Je, ni lini barabara ya Haydom kwenda Mogitu - Katesh itajengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 6

MHE. HAMISI S. TALETALE: Mheshimiwa Spika, ahsante, je, ni lini Serikali itaenda kujenga barabara ya Bigwa – Kisaki ya kilometa 78 kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Taletale, Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Mbunge atakubaliana nami kwamba barabara ilishatangazwa kwa ajili ya kuijenga na kwa hiyo sasa hivi ipo kwenye hatua ya manunuzi kwa ajili ya kuijenga kwa kiwango cha lami, ahsante.

Name

Kasalali Emmanuel Mageni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sumve

Primary Question

MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza: - Je, ni lini barabara ya Haydom kwenda Mogitu - Katesh itajengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 7

MHE. KASALALI E. MAGENI: Mheshimiwa Spika, nashukuru. Barabara ya kutoka Haydom mpaka Katesh ni mwendelezo wa barabara ya kutokea Fulo au Bujingwa kupitia Nyambiti mpaka Mari ambayo imekuwa ikiahidiwa kujengwa kwa kiwango cha lami na Serikali kwenye ilani mbalimbali za uchaguzi; je, ni lini sasa barabara hii inaanza kujengwa?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante, kama nilivyosema barabara hii iko kwenye mpango wa kuijenga; kwa hiyo mara fedha itakapokuwa imepatikana barabara hii sasa tutaanza kuijenga kama tulivyoahidi.

Name

Samweli Xaday Hhayuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hanang'

Primary Question

MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza: - Je, ni lini barabara ya Haydom kwenda Mogitu - Katesh itajengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 8

MHE. SAMWELI X. HHAYUMA: Mheshimiwa Spika, kwa kuwa wananchi maneno ya usanifu wa kina au upembuzi yakinifu hawayaelewi vizuri;

Je, ni lini Serikali itajenga barabara ya Mogitu – Hydom kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, swali lililoulizwa na Mheshimiwa Hhayuma lilikuwa ndilo swali la msingi lililohusu Mogitu – Haydom na nimeshalijibu kwamba tayari mkandarasi yupo anafanya usanifu wa hiyo barabara tujue gharama halafu fedha itafutwe kwa ajili ya kuijenga, ahsante.

Name

Seif Khamis Said Gulamali

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manonga

Primary Question

MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza: - Je, ni lini barabara ya Haydom kwenda Mogitu - Katesh itajengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 9

MHE. SEIF K. GULAMALI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana; je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa lami barabara ya Choma – Ziba – Nkinga – Simbo mpaka Puge?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara ya Choma – Puge ni barabara ambayo Mheshimiwa Mbunge amekuwa anaifuatilia sana. Hata hivyo, kwa kuwa bajeti bado hatujaiwasilisha naomba Mheshimiwa awe na subira tuone nini mwaka huu tutakuwa tumeipangia hiyo barabara.