Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 1 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 9 2023-04-04

Name

Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza: -

Je, ni lini barabara ya Haydom kwenda Mogitu - Katesh itajengwa kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Flatei Gregory Massay, Mbunge wa Mbulu Vijijini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwa kutambua umuhimu wa barabara hii, Wizara kupitia TANROADS tayari imeingia mkataba na mhandisi mshauri wa kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina, kufanya tathmini ya athari za kimazingira na uandaaji wa nyaraka za zabuni kwa ajili ya ujenzi kwa kiwango cha lami kwa barabara ya Haydom – Katesh yenye urefu wa kilometa 70. Kazi ya Usanifu imeanza mwezi Februari, 2023 na inategemewa kukamilika mwezi Februari, 2024. Baada ya usanifu kukamilika na gharama za ujenzi kujulikana, Serikali itatafuta fedha za kuanza ujenzi, ahsante.