Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Bahati Khamis Kombo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

House of Representatives

Primary Question

MHE. BAHATI KHAMIS KOMBO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itafanya ukarabati wa Jengo la Kituo cha Polisi Kengeja?

Supplementary Question 1

MHE. BAHATI KHAMIS KOMBO: Mheshimiwa Spika, ahsante, kwa kuwa Mheshimiwa Waziri amekiri kuwa kituo hiki hakiwezi kutoa huduma; je, ni mpango gani wa dharura ambao wameuweka ili kulinusuru lile jengo pamoja na wafanyakazi walioko pale?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Bahati Khamis Kombo kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, mpango wa dharura ambao tumekuwa nao ni kutumia Kituo cha Polisi cha jirani cha Mtambile iwapo wataona jengo lile linazidi kuwa hatarishi kwa watumiaji.

Mheshimiwa Spika, lakini tumebaini kuwa kituo hiki kiko umbali wa kilometa nane kutoka pale mkoani; kwa hiyo tutakachofanya ni kuharakisha kujenga kituo hiki mara baada ya bajeti yetu kupitishwa mwezi Julai ili huduma zianze kutolewa kwenye kituo ambacho ni salama zaidi.

Name

Minza Simon Mjika

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BAHATI KHAMIS KOMBO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itafanya ukarabati wa Jengo la Kituo cha Polisi Kengeja?

Supplementary Question 2

MHE. MINZA S. MJIKA: Mheshimiwa Spika, ahsante, je, ni lini Serikali itakarabati majengo ya Kituo cha Polisi Maswa ili yaweze kuendana na hadhi ya Wilaya?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge kutoka Mkoa wa Simiyu kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba Kituo cha Polisi cha Wilaya ya Maswa kweli ni cha siku nyingi na kimechakaa. Maelekezo yetu kwa IGP na wasaidizi wake kule mikoani wafanye tathmini ya kiwango cha uchakavu na kubaini gharama zinazohitajika ni kiasi gani ili kiweze kupangiwa matengenezo kadiri tutakavyopata fedha.

Name

Salma Rashid Kikwete

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mchinga

Primary Question

MHE. BAHATI KHAMIS KOMBO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itafanya ukarabati wa Jengo la Kituo cha Polisi Kengeja?

Supplementary Question 3

MHE. SALMA R. KIKWETE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, kwa kuwa Mheshimiwa Naibu Waziri alikuja Jimboni kwangu Mchinga na kuona hali halisi ya Kituo kile cha Mchinga na Gereza la Kingurungundwa; je, ni lini vituo vile vitajengwa?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Salma Rashid Kikwete kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, tunakiri kwamba Kituo cha Mchinga na Gereza la Kingurungungwa kama alivyotaja ni chakavu sana na tayari tumeingiza kwenye mpango wa bajeti wa mawaka 2023/2024. Mara tutakavyoidhinisha bajeti, fedha zimetengwa kwa ajili ya ukarabati wa Kituo cha Mchinga na ujenzi actually wa kituo kipya na ukarabati wa Gereza la Kingurungundwa.

Name

Omar Ali Omar

Sex

Male

Party

ACT

Constituent

Wete

Primary Question

MHE. BAHATI KHAMIS KOMBO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itafanya ukarabati wa Jengo la Kituo cha Polisi Kengeja?

Supplementary Question 4

MHE. OMAR ALI OMAR: Mheshimiwa Spika, ahsante sana; nami nataka niulize swali moja la nyongeza.

Mkoa wa Kaskazini Pemba kituo cha polisi kiko katika hali mbaya; je, Serikali inampango gani wa kukitengeneza kituo hicho?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Omar Omar kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli nilitembelea Pemba na nilibaini kituo kile kweli ni chakavu. Kinachotia faraja ni kwamba mkoa umeshabaini eneo la kujenga kituo kipya cha ngazi ya mkoa. Katika bajeti yetu ya mwaka ujao ni mpango wa Serikali kuanza ujenzi wa Kituo kipya cha Polisi cha Mkoa wa Kaskazini Pemba.