Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 1 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 8 2023-04-04

Name

Bahati Khamis Kombo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

House of Representatives

Primary Question

MHE. BAHATI KHAMIS KOMBO aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itafanya ukarabati wa Jengo la Kituo cha Polisi Kengeja?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Bahati Khamis Kombo, Mbunge toka Baraza la Wawakilishi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Jengo la kituo cha Polisi Kengeja, Mkoa wa Kusini Pemba ni chakavu na halifai kwa matumizi ya kutoa huduma za Kipolisi. Makadirio ya gharama za kujenga kituo kipya cha Polisi daraja C yamefanyika ambapo kiasi cha shilingi 292,544,139 zitahitajika. Fedha hizo zitaombwa kutoka mfuko wa tuzo na tozo ili ujenzi wake uanze katika mwaka wa fedha 2023/2024.