Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Janeth Maurice Massaburi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JANETH M. MASSABURI aliuliza:- Je, ni lini Serikali itatunga Sheria kali za kudhibiti madereva wasiofuata sheria za usalama barabarani?

Supplementary Question 1

MHE. JANETH M. MASSABURI: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu ya Serikali, nina maswali mawili ya nyongeza. Kwa kuwa moja ya sababu inayosababisha ajali nyingi hapa nchini ni wembamba wa barabara zetu, Je, Serikali haioni haja ya kuruhusu magari makubwa ya mizigo kutembea nyakati za usiku? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili; je, ni umri upi unaoruhusiwa kutoa leseni kwa madereva wa magari makubwa? Ahsante.

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali ya nyongeza ya Mheshimiwa Janeth Massaburi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, moja, kuhusu wembamba wa barabara; ni kweli taarifa za utafiti zinaonesha wembamba wa barabara ni moja ya sababu inayosababisha ajali na hili linafanyiwa kazi na wenzetu wa Uchukuzi na Usafirishaji, ambao ni Wajumbe wa Baraza la Taifa la Usalama barabarani na ndio maana mtaona wakati mwingine tunapanua barabara kule upande wa Mbeya na maeneo mengine inavyoonekana imekuwa changamoto.

Mheshimiwa Spika, kuhusu swali la pili, magari ya mizigo yatembee usiku; nadhani sio suluhisho la kudumu kwa sababu tunataka nchi yetu ichangamke kwenye biashara, hatuwezi kuacha kusafirisha wakati wote tukisubiri wakati wa usiku tu.

Mheshimiwa Spika, tunachotakiwa kufanya ni kuimarisha usimamizi wa sheria za usalama barabarani na kuboresha miundombinu ya barabara ili kuwe na usalama wakati wote.

Mheshimiwa Spika, kuhusu umri unaofaa kwa mtu kupewa leseni ya kuendesha magari ya mizigo ni mtu mzima, na kwa Tanzania mtu mzima baada ya miaka 18 amefanya mafunzo na amefuzu kwa vigezo vyote anaweza akapewa leseni ya kuendesha magari.

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. JANETH M. MASSABURI aliuliza:- Je, ni lini Serikali itatunga Sheria kali za kudhibiti madereva wasiofuata sheria za usalama barabarani?

Supplementary Question 2

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Katika Mji wetu wa Dar es Salaam kumejengwa barabara ya njia nane, lakini madereva wengi hawajui matumizi ya barabara ile.

Je, ni lini Serikali itaendesha mafunzo ya kutumia ile barabara kwa sababu unakuta guta limekaa kwenye highway badala ya kukaa kwenye barabara ya upande wa kushoto. Je, Serikali ni lini itatoa mafunzo rasmi?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Zuberi Kuchauka kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama Wabunge wanafuatilia na wananchi kwa ujumla kazi inayofanywa na chombo chetu cha usalama barabarani (traffic police) wanatoa elimu kupitia vyombo vya habari kuhusu usafiri kwenye kipindi cha UBA, usafiri na uraia Tanzania. Pale hutoa mafunzo mbalimbali juu ya namna barabara zile zinavyotakiwa kutumika. Kwa gari yoyote inayokwenda mwendo mdogo au inaelekea kusimama inatakiwa itembee kushoto zaidi na gari ambayo inakwenda haisimami kwenye vituo vya karibu inatakiwa ipite kule kule ambako wanaita highway. Kwa hiyo elimu hii itaendelea kutolewa ili kuwe na matumizi sahihi ya barabara hizi, nashukuru.