Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 1 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 7 2023-04-04

Name

Janeth Maurice Massaburi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JANETH M. MASSABURI aliuliza:-
Je, ni lini Serikali itatunga Sheria kali za kudhibiti madereva wasiofuata sheria za usalama barabarani?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Janeth Maurice Massaburi, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Sheria ya Usalama Barabarani, sura 168 ya mwaka 1973 kama ilivyofanyiwa marejeo mwaka 2002 na kanuni zake, inayotumika Tanzania Bara, na Sheria ya Usafiri Barabarani, Sura ya 7 ya mwaka 2003 na kanuni zake, inayotumika Zanzibar, zinatoa adhabu kwa wale wanaokiuka Sheria ya Usalama Barabarani. Serikali inaendelea kuboresha Mswada wa Marekebisho ya Sheria ya Usalama barabarani ambao tayari ulishasomwa kwa mara ya kwanza hapa Bungeni ili kuzingatia mabadiliko yaliyotokea na mahitaji ya sasa.

Mheshimiwa Spika, nashukuru.