Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hassan Zidadu Kungu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Primary Question

MHE. HASSAN Z. KUNGU aliuliza: - Je, ni lini Mradi wa REA II utakamilika katika Vijiji 23 vilivyobaki vya Jimbo la Tunduru Kaskazini?

Supplementary Question 1

MHE. HASSAN Z. KUNGU: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali, lakini nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza, niishukuru na kuipongeze Serikali kwamba imeongeza kilometa mbili za usambazaji wa umeme katika kila kijiji na kuifanya kilometa tatu badala ya kilometa moja; je, ni lini sasa Serikali itaanza utekelezaji huo wa kujazilizia kilometa mbili ili kila kijiji kipate kilometa tatu za usambazaji wa umeme? (Makofi)

Mheshimiwa Spika,swali la pili, kwa kuwa mradi huu wa REA vijijini ni mradi wa umeme vijijini; je, ni lini sasa Serikali itapeleka umeme vitongojini? Ahsante.

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Kungu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwenye swali la kwanza ni kweli Serikali ya Awamu ya Sita iliongeza kilometa mbili kwa kila kijiji ambacho kipo katika Mradi wa REA III Round Two ambao unaoendelea kutekelezwa. Kazi iliyofanyika ni kupitia maeneo yale ya vitongoji na kuyabaini ili hizo kilometa mbili zionekane wapi zipelekwe.

Mheshimiwa Spika, ninavyozungumza majadiliano na wakandarasi yanaendelea na tunaamini kuanzia mwanzoni mwa wiki inayokuja hiyo mikataba ya adendum mikataba ya nyongeza ya kupeleka umeme kwenye hizo kilometa mbili itasainiwa na hivyo tunatarajia mwanzoni mwa mwezi wa tano wakandarasi wataingia site kuendelea sasa na hiyo kazi ya kupeleka umeme katika hizo kilometa mbili za nyongeza ambazo zinatakiwa ziongezwe.

Mheshimiwa Spika, kwenye swali la pili kwamba ni lini umeme utapelekwa vitongojini. Nipende kusema hata sasa umeme unapelekwa kwenye vitongoji, Miradi ya rea inapeleka umeme vijijini ambapo vijiji vinaenda kwenye vitongoji, lakini upo mradi maalum wa densification 2B ambao unaendelea katika vijiji karibu 1,600 na wakandarasi tayari wameripoti site na wanapeleka umeme katika maeneo hayo.

Mheshimiwa Spika, lakini kubwa zaidi Serikali ipo katika taratibu za mwisho za kutafuta fedha kupeleka umeme kwenye vitongoji karibu 6101 ambavyo bado havijapata umeme na inahitajika takribani shililingi trilioni 6.5 ambayo tunaamini tutaipata kwa mbinu ambazo tayari tumepeleka maombi yetu Serikalini na mchakato wa kutafuta pesa hiyo unaendelea. Hivyo katika miaka minne mitano tunatarijia kuwa tumemaliza vitongoji vyote ambavyo havina umeme na huo ndio mpango wa Awamu ya Sita.

Name

Abubakar Damian Asenga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilombero

Primary Question

MHE. HASSAN Z. KUNGU aliuliza: - Je, ni lini Mradi wa REA II utakamilika katika Vijiji 23 vilivyobaki vya Jimbo la Tunduru Kaskazini?

Supplementary Question 2

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA: Mheshimiwa Spika, Je, ni lini Wizara itatekeleza maelekezo ya Mhesimiwa Waziri January Makamba kwa kurejesha bei ya kuunganisha umeme kwa Tarafa ya Ifakara mathalani maeneo yote yale ambayo yana asili ya vijiji 27000 kwa mfano Katinduka B na C.

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Asenga, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, utaratibu wa kubaini maeneo ya kupelekea umeme kwa gharama ndogo ulifanyika lakini haukuwa makini vya kutosha kwa hiyo tumewaelekeza wenzetu wa TANESCO warudie zoezi hilo tena kwa kuwa - consult Waheshimiwa Wabunge wote ili tupate maeneo hayo na kuyafanyia kazi sahihi.

Name

Timotheo Paul Mnzava

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Korogwe Vijijini

Primary Question

MHE. HASSAN Z. KUNGU aliuliza: - Je, ni lini Mradi wa REA II utakamilika katika Vijiji 23 vilivyobaki vya Jimbo la Tunduru Kaskazini?

Supplementary Question 3

MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru, ni upi mkakati wa Serikali kuhakikisha unaharakisha na kukamilisha kupelekwa kwa umeme kwenye vijiji vya Wilaya ya Korogwe kwa sababu mkandarasi wake anasuasua sana. (Makofi)

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mnzava, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli mkandarasi anayepeleka umeme kwenye Wilaya ya Korogwe pamoja na nyingine mbili anazembea sana na tumekubaliana achukuliwe hatua na itakapofika katikati ya mwezi huu kama atakuwa hajafikia yale makubaliano tuliyofikia basi hatua stahiki zitachukuliwa ikiwemo pamoja na kuvunja mkataba wake ambao ameshindwa kuutekeleza kwa wakati.

Name

Francis Kumba Ndulane

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kaskazini

Primary Question

MHE. HASSAN Z. KUNGU aliuliza: - Je, ni lini Mradi wa REA II utakamilika katika Vijiji 23 vilivyobaki vya Jimbo la Tunduru Kaskazini?

Supplementary Question 4

MHE. FRANCIS K. NDULANE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kuniona; je, ni lini Serikali itapeleka huduma ya umeme wa REA katika Kijiji cha Tilawandu ambacho kilisahaulika katika awamu zilizopita za utekelezaji wa umeme wa REA? (Makofi)

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu naomba kujibu naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Francis Ndulane, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, vijiji vyote ambavyo vilikuwa havina umeme vipo katika mradi wa REA Awamu ya III Mzunguko wa Pili na kwa sasa tuna takribani vijiji 2,600 tu ambavyo vimebaki havina umeme kabla ya Desemba vitakua vyote vimepata umeme.

Name

Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Primary Question

MHE. HASSAN Z. KUNGU aliuliza: - Je, ni lini Mradi wa REA II utakamilika katika Vijiji 23 vilivyobaki vya Jimbo la Tunduru Kaskazini?

Supplementary Question 5

MHE. JOSEPH M. MKUNDI: Mhesimiwa Spika, nashukuru, ni, lini Serikali itakamilisha usambazaji umeme kwenye visiwa vidogo vilivyoko nje ya Gridi ya Taifa Jimboni Ukerewe? Nashukuru.

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa ya Mheshimiwa Joseph Mkundi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, tumeshatangaza zabuni tayari kwa ajili ya wapelekaji wa umeme katika maeneo ambayo hayajafikiwa na Gridi na kinachofanyika sasa ni mchakato wa kubaini bei na uhalisia wa huduma yao ili tuweze kufikisha umeme katika maeneo ambayo Gridi ya Taifa haijafika.

Name

Nicodemas Henry Maganga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbogwe

Primary Question

MHE. HASSAN Z. KUNGU aliuliza: - Je, ni lini Mradi wa REA II utakamilika katika Vijiji 23 vilivyobaki vya Jimbo la Tunduru Kaskazini?

Supplementary Question 6

MHE. NICODEMAS H. MAGANGA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi. Vijiji 34 Mbogwe havijawekewa umeme kabisa, ni lini vitawekewa umeme, vijiji vya Mbogwe ambavyo havijapata umeme toka dunia iumbwe? (Makofi)

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Maganga, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, vijiji vyote ambavyo havina umeme viko katika mradi wa REA III Round Two na tunaendelea kusimamia na wakandarasi kuhakikisha kabla ya Disemba hii kukamilika basi vijiji vyote vimepata umeme kwa mujibu wa mikataba yetu.

Name

Ally Anyigulile Jumbe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyela

Primary Question

MHE. HASSAN Z. KUNGU aliuliza: - Je, ni lini Mradi wa REA II utakamilika katika Vijiji 23 vilivyobaki vya Jimbo la Tunduru Kaskazini?

Supplementary Question 7

MHE. ALLY A. J. JUMBE: Mheshimiwa Spika, ETBICO ni Kampuni ambayo inasambaza umeme Mkoani Mbeya, wanaenda vijijini, kwa mfano Kijiji cha Bukunelo, Kijiji cha Ikama wanasema wamewasha umeme na taarifa Serikalini ni kwamba imewasha umeme, wakati huo wamewasha transformer zinaunguruma na umeme wenyewe kwa wananchi haujafika, je hiyo ni sahihi? (Makofi)

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Ally Jumbe, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kuwasha umeme kwa mwananchi ni kumwashia katika nyumba yake na eneo lake analohitaji umeme. Kwa hiyo, kama wanasema wamewasha kwenye transformer hiyo sio sawa na tutalifuatilia kuhakikisha kwamba umeme unawafikia wananchi kwa sababu ndio wanaouhitaji. (Makofi)

Name

Nicholaus George Ngassa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igunga

Primary Question

MHE. HASSAN Z. KUNGU aliuliza: - Je, ni lini Mradi wa REA II utakamilika katika Vijiji 23 vilivyobaki vya Jimbo la Tunduru Kaskazini?

Supplementary Question 8

MHE. NICHOLAUS G. NGASSA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, Kata ya Isakamariwa, Kilinginira, Kilungu, Mwamwashiga na Mtungulu mkandarasi kaweka nguzo, je, ni lini atakamilisha kuweka waya wawashe umeme? Ahsante.

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali mawili la nyongeza la Mheshimiwa Ngassa, kwamba kabla ya Disemba hii kuisha vijiji vyote na kata zote na maeneo ambayo yapo katika Mradi wa REA III Round Two yatakuwa yamewashiwa umeme.

Name

Neema Kichiki Lugangira

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HASSAN Z. KUNGU aliuliza: - Je, ni lini Mradi wa REA II utakamilika katika Vijiji 23 vilivyobaki vya Jimbo la Tunduru Kaskazini?

Supplementary Question 9

MHE. NEEMA K. LUGANGIRA: Mheshimiwa Spika, nashukuru, ni mara ya tatu au zaidi nauliza hili swali nilitaka kufahamu ni lini Mkoa wa Kagera utaunganishwa kwenye Gridi ya Taifa?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Neema Kichiki Lugangira, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, tayari fidia imeshafanyika katika njia ya kutoka Benako kuja Kyaka kwa ajili ya kupitisha umeme utakaotoka Nyakanazi na Rusumo kuja katika Mkoa wa Kagera na Serikali kupitia BADEA imepata fedha za utekelezaji wa mradi huo, kwa hiyo, siku sio nyingi mambo yataanza kufanyika katika eneo la site.