Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 1 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 6 2023-04-04

Name

Hassan Zidadu Kungu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Primary Question

MHE. HASSAN Z. KUNGU aliuliza: -

Je, ni lini Mradi wa REA II utakamilika katika Vijiji 23 vilivyobaki vya Jimbo la Tunduru Kaskazini?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nishati, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Hassan Zidadu Kungu, Mbunge wa Tunduru Kaskazini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Mradi wa Kusambaza Umeme Vijijini Awamu ya Pili ulitekelezwa na Mkandarasi LTL ambapo jumla ya vijiji 36 vya Wilaya ya Tunduru vilipatiwa umeme na mradi ulikamilika Mwaka 2015.

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) inatekeleza Mradi wa Kusambaza Umeme Vijijini Awamu ya Tatu Mzunguko wa Pili katika Jimbo la Tunduru Kaskazini ambapo unatekelezwa na Mkandarasi M/S JV Guangdong Jianneng Electric Power Engineering Co. Ltd. and White City International Contractors Ltd. unalenga kupeleka umeme katika vijiji 23.

Mheshimiwa Spika, Mkandarasi yupo katika maeneo mbalimbali ya mradi akiendelea na kazi za ujenzi wa miundombinu na kuunganisha wateja. Mradi unatarajiwa kukamilika ifikapo mwezi Desemba, 2023.