Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Saashisha Elinikyo Mafuwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hai

Primary Question

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kufanya utafiti wa sababu za kuyeyuka kwa theluji ya Mlima Kilimanjaro na kukauka kwa vyanzo vya maji?

Supplementary Question 1

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE: Mheshimiwa Spika, ahsante, hali ya Mlima wa Kilimanjaro ni mbaya sana. Swali la kwanza kwa kuwa Serikali inakusanya fedha nyingi kutokana na Mlima Kilimanjaro, ni lini Serikali itatenga fungu maalum kwa ajili ya utafiti huo aliousema na pia operation maalum ya kupanda miti katika Jimbo la Hai?

Mheshimiwa Spika, la pili, mara kadhaa nimekuwa nikiomba Fedha za CSR na sijapata majibu humu ndani. Je, Serikali haioni ipo haja ya Wizara hizi mbili ya Muungano na Mazingira pamoja na Utalii kukaa kwa pamoja na kutengeneza mkakati kwa kuhakikisha tunaondoa tatizo la mabadiliko ya tabia nchi katika Mlima Kilimanjaro? (Makofi)

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongenza ya Mheshimiwa Saasisha Elinikyo Mafuwe, Mbunge wa Hai, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, nimwambie tu Mheshimiwa kwamba tupo tayari kutenga hilo fungu lakini n kiukweli miti mingi hapa katikati ilikufa kutokana na hali ya joto, kutokana na miti kuchomwa hovyo na kukatwa hovyo. Ofisi ya Makamu Wa Rais, Muungano na Mazingira, tayari tumeshakaa kwa kushirikiana na halmashauri na taasisi za kifedha zikiwemo CRDB, NMB na kwa kushirikiana na TFS tayari tumeshaanza huo mchakato wa upandaji miti.

Mheshimiwa Spika, nimwambie pia tuna kampeni yetu ya kusoma na mti ambapo tunashirikisha wanafunzi wa awali, msingi, sekondari, vyuo na vyuo vikuu, tunawahamasisha wapande miti. Jitihada zote tulizozichukua zitafika Kilimanjaro zitafika Hai na miti itapandwa na mazingira tutayatunza.

Mheshimiwa Spika, swali la pili nimwambie kwamba tumekuwa mara kadhaa tumekuwa na Wizara ya Maliasili kwa sababu tunaamini kwamba wao ndio wenye miti kupitia TFS ya kuweza kupanda. Sisi tupo tayari kupanda miti Kilimanjaro. Lakini tumwambie tu Mheshimiwa Mbunge yeye sasa aanze kuchukuwa juhudi ya kuanzisha hiyo Kampeni, halafu sisi kwa kushirikiana na wadau wengine tutakuja tuje tuifanye Kilimanjaro iwe ya kijani na kuhakikisha kwamba miti inapandwa na mazingira yanatunzwa.

Mheshimiwa Spika, nakushukuru. (Makofi)

Name

Anne Kilango Malecela

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Same Mashariki

Primary Question

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kufanya utafiti wa sababu za kuyeyuka kwa theluji ya Mlima Kilimanjaro na kukauka kwa vyanzo vya maji?

Supplementary Question 2

MHE. ANNE K. MALECELA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kupata hii nafasi. Matukio ya kudhoofisha Mlima Kilimanjaro yanatupunguzia pride ya sisi Watanzania kwa sababu Mlima Kilimanjaro ni pride kwa nchi yetu. Hivi Serikali hamuoni kwamba kuna umuhimu wa kuweka uzito mkubwa kuyaangalia hayo matukio yanayotokea mara kwa mara ili kuurudisha mlima wetu katika hali ambayo sio ulivyo sasa? (Makofi)

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Spika, kwanza naomba nimpongeze Naibu Waziri kwa ufafanuzi mzuri na majibu mazuri ya awali lakini Mlima Kilimanjaro ni kweli ni fahari yetu sisi Watanzania na kwa mfano mwaka jana tulipokuwa na kesi ya uwakaji wa moto Mlima Kilimanjaro, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira ilifanya kazi kubwa sana na Wizara ya Maliasili na Utalii kwa sababu Mlima ule upo chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tulienda pale kama timu na kupanga mikakati mbalimbali chini ya KINAPA. Kwa hiyo, ni kweli jambo hili la Uwakaji wa moto kwa sababu tuliunda timu kwa ajili ya kufanya utafiti nini sababu ya kuwaka moto, je ni hujuma ama ni nini? Lakini jambo hilo nadhani Serikali tunaendelea vizuri na nikuhakikishie Mama Anne Kilango Malecela, sisi dhamira yetu ya dhati ni kuhakikisha Mlima Kilimanjaro unaendelea ku-survive vizuri zaidi. Lakini niwaombe sana wanachi wa Mkoa Kilimanjaro wakati tunapanda karibuni mita 3,700 pale tumegundua kuna watu wanafanya shughuli mle ya ukati wa miti na uchomaji yaani ni changamoto kubwa.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, niwaombe wananchi wote kwamba suala la kuutunza Mlima Kilimanjaro ni jukumu la kwetu sote sisi Watanzania kwa sababu linatuletea uchumi wa hali ya juu kubwa kwa hiyo tuna kila sababu kuulinda fahari hii sote kwa pamoja kwa ajili ya nchi yetu Tanzania. Ahsante sana.

Name

Prof. Patrick Alois Ndakidemi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Moshi Vijijini

Primary Question

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kufanya utafiti wa sababu za kuyeyuka kwa theluji ya Mlima Kilimanjaro na kukauka kwa vyanzo vya maji?

Supplementary Question 3

MHE. PROF. PATRICK A. NDAKIDEMI: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa fursa. Wananchi wanaoishi katika vijiji vinavyozunguka Mlima Kilimanjaro hushindwa kuripoti changamoto za kiusalama kule mlimani kama kukata miti na moto kutokana na uhaba au uhafifu wa mawasiliano. Je, Serikali ina mpango gani kusaidia kuboresha mawasiliano katika vijiji vinavyozunguka Mlima Kilimanjaro?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali moja la nyongeza la Mheshimiwa Profesa Ndakidemi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, hii changamoto kweli tumeiona, sometimes unafika wakati kunatokezea majanga ya moto na mambo mengine, wananchi wanashindwa kuweza kutoa taarifa na sisi kama Serikali tukachukua hatua kwa wakati. Nimuambie tu Mheshimiwa kwamba hili jambo tunalichukua na tunakwenda kulifanyia kazi ili matukio yakitokea tuhakikishe kwamba sisi yanatuletea taarifa mapema na tunayachukulia hatua zinazofaa kwa mujibu yaani kwa wakati unaohusika.

Mheshimiwa Spika, nakushukuru.

Name

Boniphace Nyangindu Butondo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kishapu

Primary Question

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kufanya utafiti wa sababu za kuyeyuka kwa theluji ya Mlima Kilimanjaro na kukauka kwa vyanzo vya maji?

Supplementary Question 4

MHE. BONIPHANCE N. BUTONDO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Wilaya ya Kishapu ni moja kati ya Wilaya ambazo zipo katika mkakati na mapambano ama kampeni za mabadiliko ya tabia nchi katika Kata ya Alagana pamoja na Kata ya Kiloleli, ipo miradi iliyotekelezwa hasa ya mabwawa ya mifugo ambayo kimsingi miradi hiyo imetekezwa chini ya kiwango.

Je, Mheshimiwa Waziri upo tayari kuambatana na mimi kwenda Jimboni kwangu kujenga miradi hiyo na kushauri namna bora amna namna gani ya kuweza kuirudia na kuitekeleza upya? (Makofi)

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Spika, naomba kumshukuru kaka yangu Mbunge wa Kishapu, nadhani swali lake lilikuwa linaendena na lile swali la kwanza la EBA, kwa sababu tuna Mradi wa EBA umetekelezwa katika halmashauri tano ikiwepo na Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu sasa kwa vile swali hili lilikuwa linaenda katika upande ule wa Saasisha swali la Mlima Kilimanjaro.

Mheshimiwa Spika, kiufupi niseme ni kwamba Mheshimiwa Mbunge nitaambatana na wewe tuende tukafanye kuangalia kama kuna mapungufu ya aina yoyote kuweza kuyafanyia kazi kama Serikali, ni jukumu letu kulifanya. Lakini binafsi naomba niwashukuru hawa Wabunge wa Kishapu, Wabunge wa Nzega, Wabunge wa Mkalama, Wabunge wa Mvomero na Mpwapwa katika mradi huo wameutendea haki sana kusimamia vizuri katika maeneo mbali mbali tumepata mafanikio makubwa. Kwa hiyo, Mbunge this is my commitment kwamba tutaenda pamoja kutembelea. (Makofi)