Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 1 Enviroment Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira na Muungano 5 2023-04-04

Name

Saashisha Elinikyo Mafuwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hai

Primary Question

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kufanya utafiti wa sababu za kuyeyuka kwa theluji ya Mlima Kilimanjaro na kukauka kwa vyanzo vya maji?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NCHI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Saashisha Elinikyo Mafuwe, Mbunge wa Hai, Mkoa wa Kilimanjaro, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali ya Tanzania inayo mipango na mikakati ya kuendelea kufanya utafiti wa sababu za kuyeyuka kwa theluji ya Mlima Kilimanjaro na kukauka kwa vyanzo vya maji. Kupitia Taasisi mbalimbali za ndani ya nchini, zikiwemo Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine, na Chuo Kikuu cha Nelson Mandela, vinaendelea kufanya tafiti kuhusu suala hili. Baadhi ya sababu zilizobainika kuchangia hali hiyo ni pamoja na kuongezeka kwa wastani wa joto duniani, shughuli za binadamu zinazoendelea, ukataji wa miti na uchomaji misitu ovyo.

Mheshimiwa Spika, napenda kuchukua fursa hii kuhimiza uongozi na wananchi wa Mkoa wa Kilimanjaro kuongeza jitihada za kutunza mazingira ya mlima huo kwa kudhibiti uchomaji moto ovyo na kuongeza jitihada za kuhifadhi mazingira na kupanda miti.

Mheshimiwa Spika, nakushukuru.