Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Juma Usonge Hamad

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chaani

Primary Question

MHE. JUMA USONGE HAMAD aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kukamilisha Miradi ya muda mrefu ya Mazingira na Mabadiliko ya Tabianchi inayotekelezwa Zanzibar?

Supplementary Question 1

MHE. JUMA USONGE HAMAD: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwa vile Mheshimiwa Waziri amekiri kabisa kwamba katika miradi hiyo kuna changamoto ya ucheleweshwaji; naiomba sana Serikali, kama itaridhia.

Kwa nini kwa mwaka wa fedha huu isikamilishe miradi hii kwa kutumia fedha za ndani badala ya kusubiria fedha za wahisani, ambapo hadi leo hii ni muda wa miaka mitano miradi ile haijakamilika?

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili; je, Mheshimiwa Waziri yuko tayari kufuatana nami kwenda kuiona miradi hiyo inayotelelezwa kwenye wilaya mbili ilivyosimama na bado hatma ya kukamilika miradi hiyo haijulikani? (Makofi)

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NCHI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Juma Usonge Hamad, Mbunge wa Chaani, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, miradi hii ambayo inatekelezwa Zanzibar, takribani ukiangalia miradi yote; ile ya EBARR na hii ya LDFS ni miradi ambayo kwanza fedha zake zipo, lakini ni miradi ambayo ukiiangalia muda wake wa kukamilika bado yaani haujafika, kwa sababu miradi hii ukamilikaji wake ni mpaka 2024.

Mheshimiwa Spika, nimwambie tu Mheshimiwa Usonge kwamba pamoja na kwamba miradi hii ina fedha za wahisani, lakini pia kuna fedha ambazo zinatoka kutoka Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, zinakwenda kukamilisha miradi hii. Kwa hiyo, nimwambie Mheshimiwa asiwe na hofu.

Mheshimiwa Spika, suala la kufatana naye kwenda kukagua miradi hii, nimwambie tu kwamba niko tayari, kama ambavyo nimeshaanza mara ya kwanza, tutakwenda naye kukagua miradi hii na kuona ukamilifu wake na namna ambavyo inanufaisha wananchi. Nakushukuru.