Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 1 Enviroment Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira na Muungano 4 2023-04-04

Name

Juma Usonge Hamad

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chaani

Primary Question

MHE. JUMA USONGE HAMAD aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kukamilisha Miradi ya muda mrefu ya Mazingira na Mabadiliko ya Tabianchi inayotekelezwa Zanzibar?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), naomba kujibu swali la Mheshimiwa Usonge Hamad Juma, Mbunge wa Chaani, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Ofisi ya Makamu wa Rais, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inaratibu miradi miwili kwa Upande wa Zanzibar. Mradi mmoja wa Kuhimili Mabadiliko ya Tabianchi kwa Kutumia Mifumo Ikolojia Vijijini (EBARR) unaotekelezwa kwenye Wilaya ya Kaskazini A, Unguja; na Mradi wa Kurejesha Ardhi Iliyoharibika na Kuongeza Usalama wa Chakula katika Maeneo Kame Nchini (LDFS) unaotekelezwa katika Wilaya ya Micheweni, Pemba.

Mheshimiwa Spika, katika kuhakikisha miradi hii inakamilika kwa wakati, tayari Serikali imechukua hatua za kiutendaji kuwataka waratibu na washughulikiaji wa miradi hii kitaifa kuhakikisha miradi inakamilika kikamilifu na kwa ubora. Aidha, Ofisi ya Makamu wa Rais inaendelea kuwasiliana na Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar ili kusimamamia utekelezaji wa miradi hiyo kwa upande wa Zanzibar ili miradi hii ikamilike kwa wakati.

Mheshimiwa Spika, nakushukuru.