Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Shally Josepha Raymond

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SHALLY J. RAYMOND K.n.y. MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza: - Je, ni lini Serikali italeta Sheria Bungeni kuruhusu Halmashauri kuzikopesha SACCOS za vijana na wanawake?

Supplementary Question 1

MHE. SHALLY J. RAYMOND: Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa kuwa mikopo hiyo kutokuwa na riba ni kivutio kikubwa sana kwa wale ambao hawana uwezo; na wakati huo huo wanawake wana vikoba: Je, Serikali inaonaje sasa kama wale wa vikoba watapatiwa mikopo hiyo?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Shally Raymond Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, sheria ya mikopo ya asilimia kumi imeeleza kwamba wajasiriamali wanawake, vijana na watu wenye ulemavu wanaweza kukopeshwa wakijiunga kwenye vikundi vyao na mkopo huo hauna riba. Kwa hiyo, kama wanawake walio kwenye vikoba ni sehemu ya kikundi cha wajasiriamali bila kujali kwamba wapo kwenye vikoba au la, wataweza kukopeshwa fedha hizo kwa utaratibu huo na kufanya shughuli zao ili kujiletea maendeleo, ahsante. (Makofi)

Name

Halima James Mdee

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SHALLY J. RAYMOND K.n.y. MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza: - Je, ni lini Serikali italeta Sheria Bungeni kuruhusu Halmashauri kuzikopesha SACCOS za vijana na wanawake?

Supplementary Question 2

MHE. HALIMA J. MDEE: Mheshimiwa Spika, asilimia 10 tuliipitisha kwa mabadiliko ya Sheria ya mwaka 2019, lakini Taarifa za Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kuhusiana na asilimia 10 ya mwaka 2021 zilipotea shilingi bilioni 47.5; za mwaka 2021/2022 iliyotoka juzi, zimepotea shilingi bilioni 88.

Mheshimiwa Spika, swali langu kwa Waziri; kwa kuwa Wakurugenzi ambao ndio accounting officers wamepewa majukumu ya kusimamia hizi fedha kuhakikisha zinawafikia watu sahihi, lakini Wakurugenzi hawafanyi hivyo, matokeo yake fedha nyingi zinapotea: Ni lini Serikali inapanga kuchukua hatua kali za kisheria dhidi ya accounting officers huko kwenye Halmashauri zetu wanaoshindwa kutekeleza majukumu yao?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Halima James Mdee, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli moja ya changamoto kubwa katika mikopo ya asilimia 10 ni kasi ya maejesho kwa vikundi vilivyokopeshwa. Serikali imetambua changamoto na ndiyo maana katika miaka mitatu mfululizo, kasi ya urejeshaji imetoka asilimia 62 mwaka 2018/2019 mpaka asilimia karibu 80 mwaka 2021/2022.

Mheshimiwa Spika, pamoja na changamoto hiyo Serikali imeendelea kuchukua hatua kwa accounting officers, kwa maana ya Wakurugenzi katika Halmashauri zetu ambao walithibitika kutosimamia ipasavyo marejesho ya mikopo ya asilimia kumi. Zoezi la kuchukua hatua kwa accounting officers ni endelevu. Kila mara Serikali itakapotambua kwamba kuna Mkurugenzi hajatimiza wajibu wake na fedha hazijarejeshwa, lazima atachukuliwa hatua kwa mujibu wa taratibu za utumishi na kwa mujibu wa taratibu za kisheria, ahsante.

Name

Josephine Johnson Genzabuke

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SHALLY J. RAYMOND K.n.y. MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza: - Je, ni lini Serikali italeta Sheria Bungeni kuruhusu Halmashauri kuzikopesha SACCOS za vijana na wanawake?

Supplementary Question 3

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Spika, ahsante, kwanza nampongeza Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa uamuzi wake kwamba asilimia zilizokuwa zikikopeshwa kwenye Halmashauri zipitie benki: -

Mheshimiwa Spika, sasa kwa kuwa wanawake na vijana watakuwa wanakopeshwa kupitia benki: Je, ni kwa nini sasa Serikali isiamue vikundi ambavyo ni vya wanawake na vijana vilivyounda SACCOS navyo viunganishwe katika kukopeshwa kupitia benki? (Makofi)

Name

Angellah Jasmine Mbelwa Kairuki

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Genzabuke na pia nimpongeze sana Naibu Waziri, Mheshimiwa Dkt. Dugange kwa majibu mazuri yenye umakini mkubwa sana; na niwashukuru kwa maswali yote yaliyoulizwa na Waheshimiwa Wabunge wote; Mheshimiwa Shally Raymond pamoja na Mheshimiwa Halima Mdee.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa tayari Mheshimiwa Rais ameshaelekeza kwamba tutakuwa na mfumo mpya wa utoaji wa mikopo hii ya asilimia 10, napenda tu kuwahakikishia Waheshimiwa Wabunge wenzangu kwamba tumeshaanza kuandaa utaratibu na pindi utakapokuwa tayari, tutawajulisha na tutaweza kujua katika benki tutakuwa kwa mfumo wa aina gani? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, tutaendelea kupokea maoni yoyote yatakayoboresha namna gani katika benki pia mfumo huu uweze kutumika na tunawashukuru. Kikubwa tunawaomba, kwa zile ambazo tayari zilishatolewa na zilishakopeshwa, tulishaanza kuingia mikataba na walionufaika na mikopo hii na ni azma ya Serikali kuhakikisha kwamba fedha zote ambazo zilitolewa tangu mikopo hii kuanza kutolewa zinarudishwa na ndiyo moja ya fedha hizo hizo pia tutakazozitumia katika kupeleka katika benki zetu na kuzikopesha kwa ajili ya utaratibu mpya. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, niendelee kuwasisitiza na kuwaomba Waheshimiwa Wabunge, kwa kuwa wanaingia Mabaraza ya Madiwani, kuhakikisha kwamba fedha zote zilizokopeshwa nyuma zinarudi, na pia bado tunaendelea kupokea ushauri kwamba ni namna gani tunaweza tukatekeleza vyema katika huo mfumo mpya utakaotolewa katika benki zetu.

Mheshimiwa Spika, nakushukuru. (Makofi)