Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 1 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 3 2023-04-04

Name

Josephine Johnson Genzabuke

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SHALLY J. RAYMOND K.n.y. MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza: -

Je, ni lini Serikali italeta Sheria Bungeni kuruhusu Halmashauri kuzikopesha SACCOS za vijana na wanawake?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Josephine Johnson Genzabuke, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, mikopo ya asilimia 10 inatolewa kwa mujibu wa kifungu cha 37A cha Sheria ya Fedha za Serikali za Mitaa Sura ya 290. Kifungu hicho kimeeleza kwamba Halmashauri zote zinapaswa kutenga asilimia 10 ya mapato yake ya ndani kwa ajili ya mikopo isiyo na riba kwa vikundi vilivyosajiliwa vya Wanawake, Vijana na Watu wenye Ulemavu.

Mheshimiwa Spika, mikopo ya SACCOS huendeshwa kwa Sheria ya Huduma Ndogo za Fedha (Vyama vya Ushirika wa Akiba na Mikopo) ya mwaka 2019 ambapo mikopo hiyo hutolewa kwa wanachama wa SACCOS kwa riba. Hivyo, mapendekezo ya kurekebisha Sheria ya Fedha za Serikali za Mitaa Sura ya 290 ili kuzikopesha SACCOS kutaondoa kusudio la kutoa mikopo isiyo na riba kwa wanawake, vijana na watu wenye ulemavu.