Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Pius Stephen Chaya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Mashariki

Primary Question

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA aliuliza: - Je, ni lini barabara ya kutoka Kintinku hadi Makanda inayounganisha Mkoa wa Singida na Dodoma itahamishiwa TANROADS?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri ya Serikali, ninayo maswali mawili ya nyongeza: Je, ni lini ujenzi wa Daraja la Ntumbi ambalo linaunganisha barabara ya Ntumbi - Nangongo utaanza kufanya kazi?

Mheshimiwa Spika, swali la pili: Nini mpango wa Serikali wa kuweka taa za barabarani katika Mji wa Manyoni ili kuweza kuboresha ulinzi na usalama wa Mji wa Manyoni?

Mheshimiwa Spika, nashukuru sana.

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Dkt. Pius Chaya, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwa daraja la Ntumbi, tayari bajeti ilikuwa imeshatengwa shilingi milioni 496 na tayari usanifu ulikuwa umeshafanyika na sasa wapo katika hatua za kutangaza ili daraja hili liweze kujengwa na wananchi wa Mheshimiwa Chaya pale na Watanzania wale wa Manyoni waweze kupata huduma ya barabara hiyo kupitika.

Mheshimiwa Spika, nikienda kwenye swali lake la pili kuhusu taa za barabarani, katika mwaka huu wa fedha tayari bajeti ilikuwa imetengwa kwa taa 15. Kwenye hili pia nampongeza Mheshimiwa Mbunge kwa kulifuatilia sana. Tayari katika bajeti ya mwaka wa fedha unaofuata zimetengwa taa 28 pale Manyoni Mjini ambapo tutaenda kutekeleza.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.

Name

Philipo Augustino Mulugo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Songwe

Primary Question

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA aliuliza: - Je, ni lini barabara ya kutoka Kintinku hadi Makanda inayounganisha Mkoa wa Singida na Dodoma itahamishiwa TANROADS?

Supplementary Question 2

MHE. PHILLIPO A. MULUGO: Mheshimiwa Spika, nashukuru nami kupata kupata nafasi hii.

Mheshimiwa Naibu Waziri vikao vya RCC Mkoa wa Songwe vimekuwa vikipitisha barabara ya kutoka Kapalala kwenda Buha kilometa 36 kila mwaka toka nimeingia Ubunge, lakini hatujawahi kupata majibu ya kwamba barabara hiyo imepandishwa hadhi. Kila wakati tunakaa tunapeleka, tukaa tunapeleka, na leo mmesema ndiyo vikao halali vinavyopitisha. Lini barabara hiyo itakuwa ya hadhi ya TANROADS?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Phillipo Mulugo kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama nilivyosema kwenye majibu yangu ya msingi, suala hili likishapitishwa kisheria kwenye vikao husika linakwenda kwa Waziri mwenye dhamana ya barabara ambaye ni Waziri wa Ujenzi. Sasa sisi kwa pamoja kwa kushirikiana na Wizara ya Ujenzi tutalifuatilia na Mheshimiwa Mbunge tutaona wapi ambapo japo hili limekwama na tutampatia majibu, lakini dhamana yake ipo kwa Waziri wa Ujenzi.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha. (Makofi)

Name

Hussein Nassor Amar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyang'hwale

Primary Question

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA aliuliza: - Je, ni lini barabara ya kutoka Kintinku hadi Makanda inayounganisha Mkoa wa Singida na Dodoma itahamishiwa TANROADS?

Supplementary Question 3

MHE. HUSSEIN N. AMAR: Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa kuwa ujenzi wa kilomita moja ya lami Makao Makuu ya Wilaya ya Nyang’hwale pale Kalumwa, mkandarasi aliingia kwa kasi kubwa na akaweka vifusi na akashindilia; na baada ya hapo hajaweka lami; na leo zaidi ya miezi mitatu haonekani site; tatizo ni nini?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Hussein Amar, Mbunge wa Nyang’hwale kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, tutalifuatilia jambo hili, na tutawasiliana na Meneja wa TARURA wa Mkoa wa Geita na vilevile wa Wilaya ya Nyang’hwale kujua ni kwa nini mkandarasi huyu amekwama kuendelea na kazi hii? Vilevile nitakutana na Mheshimiwa Mbunge tuweze kulitafutia majawabu leo hii hii hapa tukiwa katika viwanja vya Bunge. (Makofi)

Name

Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA aliuliza: - Je, ni lini barabara ya kutoka Kintinku hadi Makanda inayounganisha Mkoa wa Singida na Dodoma itahamishiwa TANROADS?

Supplementary Question 4

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Je, ni lini barabara ya kuanzia Mzumbe kibaoni kwenda mpaka Lubungo mpaka Kibambila ambayo ni Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero, mpaka Kimamba, Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa itajengwa na kupitika kwa mwaka mzima kwa kuunganisha wilaya zote mbili? Ahsante.

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ishengoma, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, tutalifuatilia suala hili kwa kuona barabara hii kama imetengewa bajeti katika mwaka huu wa fedha tunaokwenda. Nafahamu Waziri wa Nchi, Mheshimiwa Angellah Kairuki amekaa na Waheshimiwa Wabunge wa Mikoa yote na kuangalia vipaumbele katika barabara, afya na elimu. Hivyo, tutaangalia kama barabara hii na yenyewe imo ili tuone ni namna gani ambavyo tunaweza tukawafikia wananchi hawa wa kwa Mheshimiwa Ishengoma.

Name

Ally Mohamed Kassinge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kusini

Primary Question

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA aliuliza: - Je, ni lini barabara ya kutoka Kintinku hadi Makanda inayounganisha Mkoa wa Singida na Dodoma itahamishiwa TANROADS?

Supplementary Question 5

MHE. ALLY M. KASSINGE: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kuniona kwa nafasi ya swali la nyongeza. Barabara ya kutoka Hoteli tatu mpaka Pande na hatimaye Limalyao katika Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa imeshafanyiwa mapendekezo ya kupandishwa hadhi ili iwe ya TANROADS na vikao husika. Lini Serikali itapandisha hadhi barabara hii?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ally Kassinge, Mbunge wa Kilwa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama nilivyotoa majibu ya awali kwa Mheshimiwa Mulugo na Mheshimiwa Chaya, ili kupandisha hadhi barabara hizi, baada ya mchakato wote kuwa umeshapitiwa, sasa ni mamlaka ya Waziri mwenye dhamana ya barabara ni Waziri wa Ujenzi. Sasa wakati tunafuatilia suala la Mheshimiwa Mulugo tutahakikisha na hili la Mheshimiwa Kassinge nalo tunaliangalia.

Name

Dr. Christina Christopher Mnzava

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA aliuliza: - Je, ni lini barabara ya kutoka Kintinku hadi Makanda inayounganisha Mkoa wa Singida na Dodoma itahamishiwa TANROADS?

Supplementary Question 6

MHE. DKT. CHRISTINA C. MNZAVA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa barabara ya kutoka Kolandoto kwenda Kishapu ni barabara muhimu sana kwa uchumi wa Kishapu: Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa kiwango cha lami? (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mnzava, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali hii ya Awamu ya Sita ya Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, imeweka kipaumbele sana katika kuhakikisha barabara zetu zinapitika wakati wote ikiwemo barabara hii ya Kolandoto kwenda Kishapu. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, tutaliangalia suala hili na kuona ni namna gani barabara hii nayo itaweza kuwekewa fedha na kuweza kutengenezwa.