Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 1 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 2 2023-04-04

Name

Dr. Pius Stephen Chaya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Mashariki

Primary Question

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA aliuliza: -

Je, ni lini barabara ya kutoka Kintinku hadi Makanda inayounganisha Mkoa wa Singida na Dodoma itahamishiwa TANROADS?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Pius Stephen Chaya, Mbunge wa Jimbo la Manyoni Mashariki, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Sheria ya Barabara Na. 13 ya mwaka 2007, kifungu cha 11 na Kanuni za Usimamizi wa Barabara ya mwaka 2009 kifungu 43(1) na (2) na kifungu 44(1) kupitia Tangazo la Serikali Na. 21 ya tarehe 23 Januari 2009, zimeainisha vigezo na utaratibu wa kuhamisha barabara ili iwe chini ya TANROADS ambapo barabara inaweza kupandishwa au kuteremshwa toka daraja moja kwenda daraja lingine.

Mheshimiwa Spika, suala la kupandisha hadhi barabara ni la kisheria na kuzingatia vigezo. Ili barabara iweze kupanda kutoka daraja la barabara ya Wilaya kwenda daraja la barabara ya Mkoa (kusimamiwa na TANROADS) inatakiwa barabara hiyo ijadiliwe kwenye Kikao cha Bodi ya Barabara ya Mkoa husika na ikionekana inakidhi vigezo, Bodi hiyo kupitia kwa Mwenyekiti itamshauri Waziri mwenye dhamana na barabara kuwa barabara husika imekidhi vigezo na hivyo ipandishwe daraja na kuwa chini ya TANROADS.

Mheshimiwa Spika, hivyo, nashauri utaratibu wa kuhamisha barabara kwenda TANROADS uzingatiwe ikiwemo kwa hii ya Kintinku - Makanda kwenda TANROADS.