Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Antipas Zeno Mgungusi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Malinyi

Primary Question

MHE.ANTIPAS Z. MGUNGUSI aliuliza: - Je, Serikali haioni haja ya kurekebisha utaratibu wa kuwaachia makusanyo ya fedha Jeshi la Uhifadhi hasa TANAPA?

Supplementary Question 1

MHE. ANTIPAS Z. MGUNGUSI: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa majibu ya Serikali ambayo sijaridhika sana. Kimsingi nilitarajia nijibiwe swali na Wizara ya Fedha, lakini hamna shida kwa sababu Serikali ni moja. Ilikuwa ni nia njema ya Serikali kuokoa Jeshi la Uhifadhi kwa maana ya kufanya operesheni zake kutokana na uwezo wao mdogo wa kuingiza mapato kipindi cha COVID. Sasa hivi kuna jitihada mbalimbali ambazo zinafanywa na Serikali hasa Mheshimiwa Rais katika kuifungua nchi. Tunatarajia wageni watakuwa wengi na Jeshi la Uhifadhi litaweza kujiimarisha. Je, Serikali haioni haja sasa kubadilisha sheria ili TANAPA na TAWA waweze kukusanya fedha zao wenyewe na kuendelea kupeleka gawio Serikalini?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Antipas Mgungusi, Mbunge wa Malinyi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwenye jibu la msingi nimesema wazi kabisa kwamba ni vyema fedha yote inapokusanywa ikaingia kwenye kapu moja ili kuona hata vyanzo vyetu vya mapato tunapataje. Pamoja na yote hayo maelezo yangu yalikuwa ni kwamba kipindi hiki ambacho sasa tumeanza kuimarika, bado tunachechemea, nikimaanisha kwamba Serikali bado inalisaidia hili Shirika la Uhifadhi (TANAPA). Kwa hiyo tutakapofikia mahali ambapo tunasimama wenyewe basi Serikali itaona kama kuna haja ya kubadilisha sheria tutaleta ndani ya Bunge lako Tukufu na sheria itaendelea kurekebishwa. Ahsante.

Name

Emmanuel Peter Cherehani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Primary Question

MHE.ANTIPAS Z. MGUNGUSI aliuliza: - Je, Serikali haioni haja ya kurekebisha utaratibu wa kuwaachia makusanyo ya fedha Jeshi la Uhifadhi hasa TANAPA?

Supplementary Question 2

MHE. EMMANUEL P. CHEREHANI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kuniona. Mgogoro kati ya Pori la Usumbwa Forest Reserve na Pori la Hifadhi ya Taifa Kigosi Moyowosi umedumu kwa muda mrefu sana. Sasa je, ni lini Serikali itaushughulikia mgogoro huu ili kuwapa nafasi wananchi wa Jimbo la Ushetu hasa wanaozunguka Kata za Idahina, Nyankende, Ulewe pamoja na Ubago waendelee na shughuli zao?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Cherehani, Mbunge wa Ushetu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, awali ya yote niendelee kuwaomba wananchi ambao wanaishi kwenye maeneo haya waendelee kuwa na subira wakati Serikali inaendelea kuangalia namna iliyo bora ya kutatua migogoro hii.

Mheshimiwa Spika, tuna Kamati ya Mawaziri Nane ambayo ina maelekezo kutoka kwa Mheshimiwa Rais kwamba tuzunguke nchi nzima kuhakikisha kwamba tunatatua migogoro hiyo. Sambamba na hilo tumezielekeza taasisi, endapo kuna migogoro mipya ambayo haimo ndani ya hii migogoro inayotatuliwa na Kamati ya Mawaziri Nane basi tuanze pia kuangalia mchakato mpya kuangalia namna iliyo bora ili tuweze kutatua migogoro hiyo. Kwa hiyo, niwaombe wananchi wote ambao wana migogoro mipya katika maeneo yao Serikali inaendelea kuyafanyia kazi ili tuone njia iliyo bora ya kutatua migogoro hiyo.

Name

Dr. Charles Stephen Kimei

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vunjo

Primary Question

MHE.ANTIPAS Z. MGUNGUSI aliuliza: - Je, Serikali haioni haja ya kurekebisha utaratibu wa kuwaachia makusanyo ya fedha Jeshi la Uhifadhi hasa TANAPA?

Supplementary Question 3

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa nafasi hii, nina swali dogo gu. Kwa vile Serikali imetuhakikishia kwamba Mamlaka za Hifadhi za Misitu na Wanyamapori wana wajibu wa kutoa CSR kwa vijiji vinavyozunguka hifadhi hizi. Je, Mheshimiwa Waziri yuko tayari kuziagiza mamlaka hizi ziweke bayana kiasi cha ufadhili ambazo zimetolewa kwa vijiji hivyo ndani ya miaka mitatu iliyopita? (Makofi)

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kimei, Mbunge wa Vunjo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, awali ya yote niwaombe sana wananchi wanaozunguka maeneo ya hifadhi waamini kwamba Serikali inatambua umuhimu wa mashirikiano ikiwemo miradi ya ujirani mwema.

Mheshimiwa Spika, bajeti zote tunapozileta hapa Bungeni huwa tunaweka kipengele cha miradi ya CSR. Nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba hata bajeti hii tutakayoisoma hivi karibuni itazingatia hilo. Hivyo, niwaombe wananchi wote na Waheshimiwa Wabunge ambao wanazungukwa na maeneo haya yaliyohifadhiwa watarajie kuona CSR katika maeneo yao. Ahsante sana.

Name

Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Primary Question

MHE.ANTIPAS Z. MGUNGUSI aliuliza: - Je, Serikali haioni haja ya kurekebisha utaratibu wa kuwaachia makusanyo ya fedha Jeshi la Uhifadhi hasa TANAPA?

Supplementary Question 4

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi. Jitihada za Serikali ni pamoja na kuhakikisha kwamba mapato yatokanayo na utalii yanaendelea kuongezeka kwa kuboresha miundombinu na kufanya marketing ya utalii. Je, ni lini Serikali itaanza utekelezaji kikamilifu wa Mradi wa REGROW ambao ulizinduliwa tarehe 12 Februari, 2018 na Mheshimiwa Makamu wa Rais ambaye sasa ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Chumi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Mradi wa REGROW ulianza kutekelezwa mwaka 2017, lakini kutokana na changamoto ambazo zilijitokeza, Benki ya Dunia iliweza kuongeza muda mpaka mwaka 2025, ambapo tutamaliza mradi huu. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Wizara imeunda Kamati Maalum ambayo itafanya kazi bega kwa bega kuhakikisha eneo hili tunasimamia vizuri kama ambavyo tunasimamia fedha za UVIKO ili kuhakikisha mradi huu unakamilika haraka na kuhamasisha watalii waweze kufika katika maeneo hayo. Ahsante.