Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 24 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 211 2022-05-17

Name

Antipas Zeno Mgungusi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Malinyi

Primary Question

MHE.ANTIPAS Z. MGUNGUSI aliuliza: -

Je, Serikali haioni haja ya kurekebisha utaratibu wa kuwaachia makusanyo ya fedha Jeshi la Uhifadhi hasa TANAPA?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Antipas Zeno Mgungusi, Mbunge wa Malinyi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, awali ya yote napenda kupongeza Serikali ya Awamu ya Tano na Sita kwa kuendelea kutekeleza takwa la kisheria la kuhakikisha makusanyo yote yanaingia kwenye kapu moja (Mfuko Mkuu wa Serikali). Katika kuendelea kutekeleza takwa hilo, Serikali ilibadili Sheria ya Fedha ya mwaka 2020 ambapo jukumu la kukusanya mapato yasiyo ya kodi ikiwemo ya Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) lilikasimiwa kwa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).

Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha mwaka 2019/2020, mapato ya Jeshi la Uhifadhi (TANAPA) yalishuka kutokana na kushuka kwa ukusanyaji wa mapato kulikosababishwa na kupungua kwa wageni kufuatia makatazo ya kusafiri na kufungiwa (lockdown) baada ya kuibuka kwa janga la UVIKO-19. Hii ilisababisha Jeshi la Uhifadhi (TANAPA) kushindwa kumudu gharama mbalimbali za uendeshaji.

Mheshimiwa Spika, kutokana na changamoto hizo za kimapato, Serikali iliamua kugharamia shughuli zote za uhifadhi ikiwemo kulipa mishahara ya watumishi na kutoa ruzuku ya kugharamia matumizi ya kawaida na miradi ya maendeleo. Aidha, katika kuhakikisha Jeshi la Uhifadhi (TANAPA) halikwami katika utekelezaji wa majukumu yake kwa wakati, Serikali imekuwa ikitoa fedha za matumizi kwa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) miezi miwili kabla yaani advance disbursement. Hata hivyo, Serikali itaendelea kufanyia kazi hoja ya Mheshimiwa Mbunge wakati ikiendelea na utaratibu huu hadi hapo itakapoona kama kuna uhitaji wa kubadilisha Sheria.