Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Omar Issa Kombo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wingwi

Primary Question

MHE. OMAR ISSA KOMBO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Ofisi ya Posta katika Wilaya ya Micheweni?

Supplementary Question 1

MHE. OMAR ISSA KOMBO: Mheshimiwa Spika, ahsante, kwa kweli nimpongeze sana Mheshimiwa Waziri kwa majibu yake mazuri. Kwa kweli ni matumaini yangu kwamba wananchi wa Micheweni watafarajika pindi watakaposikia majibu haya ya Serikali.

Mheshimiwa Spika, pamoja na pongezi hizo nina swali moja la nyongeza. Mara nyingi imezoeleka katika Shirika la Posta wakati wanapotoa ajira wanachukua waajiriwa kutoka katika maeneo mengine. Je, Mheshimiwa Waziri ananihakikishiaje, pindi watakapofungua ofisi hii katika ajira ambazo watatoa watazingatia kipaumbele au wataweka kipaumbele kwa wananchi wa Wilaya ya Micheweni?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Omar Issa Kombo, Mbunge wa Wingwi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza kabisa naomba nichukue fursa hii kumshukuru sana Mheshimiwa Mbunge kwa kazi ambayo anaifanya kwa ajili ya wananchi wa Wingwi. Lakini vilevile ameendelea kuhakikisha kwamba anatupatia changamoto zinazoendelea ndani ya jimbo lake. Sisi kama Serikali tunaendelea kuzipokea na kuzifanyia kazi.

Mheshimiwa Spika, lakini pili suala la ajira linafahamika kabisa kwamba mashirika yetu haya yanaajiri kwa kupitia utaratibu wa utumishi wa umma. Hivyo basi, tunaamini kabisa kwamba mfanyakazi yeyote, au yeyote ambaye ni Mtanzania ana haki sawa kuomba kazi na kupatiwa kazi kulingana na vigezo ambavyo vitakuwa vimewekwa.

Name

Saashisha Elinikyo Mafuwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hai

Primary Question

MHE. OMAR ISSA KOMBO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Ofisi ya Posta katika Wilaya ya Micheweni?

Supplementary Question 2

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kuniona. Baada ya uzinduzi wa Royal Tour kumekuwa na ongezeko kubwa sana la watalii ndani ya Jimbo la Hai, lakini moja ya changamoto inayoikumba sekta hii ni mawasiliano. Hoteli za kitalii zilizoko kwenye geti la kuingia Machame ambapo Naibu Waziri ameshafika hazina mawasiliano kabisa. Je, Serikali ina mpango gani wa kuleta mawasiliano ndani ya Jimbo la Hai?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Saashisha Mafuwe, Mbunge wa Hai, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni jukumu la Serikali kwa mujibu wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi, Ibara ya 61(j) inatuelekeza kuhakikisha kwamba tunafikisha mawasiliano kwa Watanzania wote. Vilevile specifically kwa maeneo ya Jimbo la Hai mimi binafsi nimeshafika katika maeneo ambayo ameyataja Mheshimiwa Mbunge na kweli kabisa tayari tumeshayachukua na tayari wataalam wameshafanya tathmini na tunayaingiza kwenye mpango wa utekelezaji wa Tanzania ya Kidigitali. Kwa hiyo naomba tuendelee kushirikiana na Mheshimiwa Mbunge kuhakikisha kwamba mawasiliano tunayafikisha huko, lakini tuwaandae wananchi wetu tutakapohitaji maeneo kwa ajili ya ujenzi wa minara hiyo, watupatie ushirikiano ili mawasiliano yaweze kufika. Ahsante.

Name

Soud Mohammed Jumah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Donge

Primary Question

MHE. OMAR ISSA KOMBO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Ofisi ya Posta katika Wilaya ya Micheweni?

Supplementary Question 3

MHE. SOUD MOHAMMED JUMAH: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Katika Jimbo langu la Donge kuna majengo ambayo yamejengwa zaidi ya miaka 20 iliyopita na wenzetu hawa wa Posta na Simu. Majengo yale mpaka leo hayakutumika na yanaendelea kuzeeka na kuchakaa hivi sasa. Sasa namwomba tu Mheshimiwa Waziri kama yuko tayari aidha tufuatane na kumwomba awaachie wananchi wa Jimbo la Donge watumie yale majengo kwa shughuli zingine za maendeleo. Ahsante.

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Soud, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Shirika la Posta Tanzania majengo yake mengi ni ya siku nyingi, lakini mpango wa uliopo ndani ya shirika letu ni kuhakikisha kwamba tunaboresha vituo vyetu vya mikoani. Kwa majengo yetu yaliyoko katika upande wa wilaya baada ya kukamilisha awamu ya kwanza ambayo ni mikoa baadaye tutashuka mpaka kwenye wilaya na hatimaye majengo yote yataanza kufanya kazi iliyotajiwa na Watanzania. Ahsante.

Name

Daniel Baran Sillo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Primary Question

MHE. OMAR ISSA KOMBO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Ofisi ya Posta katika Wilaya ya Micheweni?

Supplementary Question 4

MHE. DANIEL B. SILLO: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza swali moja dogo la nyongeza. Kwa kuwa kuna changamoto kubwa sana ya mawasiliano katika Jimbo la Babati Vijijini hasa Tarafa za Bashnet na Goroa na pia Mheshimiwa Naibu Waziri alishafika. Je, ni lini Serilkali itaanza kujenga minara ili wananchi wetu waweze kupata mawasiliano?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Daniel Sillo, Mbunge wa Babati, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza naomba nimpongeze sana Mheshimiwa Sillo kwa sababu nilifanya ziara katika jimbo lake na tulitembea wote na tulijionea hali halisi, lakini habari njema kwa ajili ya wananchi wa Babati ni kwamba kata ambazo amezitaja tayari zipo kwenye mpango wa utekelezaji wetu. Hivyo basi, wananchi wa Babati wasubiri tu hatua za manunuzi zikamilike. Hatua hizo zikishakamilika basi nimwombe Mheshimiwa Mbunge tuendelee kushirikiana kuhakikisha kwamba wananchi wetu wanatupa maeneo ambayo hayana migogoro kiasi kwamba tukiweka minara yetu isiingie kwenye migogoro ya ardhi. Ahsante sana.