Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 24 Works, Transport and Communication Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari 210 2022-05-17

Name

Omar Issa Kombo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wingwi

Primary Question

MHE. OMAR ISSA KOMBO aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itajenga Ofisi ya Posta katika Wilaya ya Micheweni?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Omar Issa Kombo, Mbunge wa Wingwi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kutokana na ukuaji wa teknolojia ya TEHAMA na mabadiliko yanayoendelea ndani ya Shirika la Posta Tanzania (TPC) katika utoaji wa huduma kwa njia za kielekitroniki kupitia mawakala, Shirika halijapanga kujenga Ofisi ya kutolea huduma bali litatumia mawakala katika kutoa na kufikisha huduma zake kwa wananchi.

Mheshimiwa Spika, Shirika la Posta Tanzania limepanga kutumia Kituo cha TEHAMA kilichopo Micheweni kinachomilikiwa na Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar ili kutoa huduma za Posta kwa wananchi wa Wilaya ya Micheweni kwa kutumia wakala. Shirika tayari limewasilisha maombi ya kupatiwa nafasi katika Kituo hicho na kukubaliwa. Shirika linakamilisha taratibu ili huduma za posta zianze kutolewa kabla ya mwaka wa fedha 2021/2022 kukamilika.