Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Jafari Chege Wambura

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rorya

Primary Question

MHE. JAFARI W. CHEGE aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka mradi wa maji safi na salama katika Kata ya Rabour?

Supplementary Question 1

MHE. JAFARI W. CHEGE: Mheshimiwa Spika, nikushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali lanyongeza. Ni kweli, nikiri kwamba mradi huu unaendelea na utakapokamilika, tuweke rekodi sawa, utanufaisha wananchi 4,792 badala ya laki moja na kidogo.

Mheshimiwa Spika, nataka niulize maswali mawili ya nyongeza pamoja na haya, kwamba wananchi wa kata ile wako zaidi ya 12,000, mradi huu ukikamilika unakwenda kuhudumia wananchi 4,700. Nataka nijue mkakati wa Serikali walionao ili kuhakikisha angalau wananchi wote waliosalia kwa zaidi ya elfu kumi na mbili na kidogo wanaweza kupata maji safi na salama?

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili, kuna kituo cha afya ambacho kinajengwa kwenye kata ile, hivi ninavyozungumza wananchi wanatafuta eneo kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha afya. Nilitaka nijue kama mpango huu wa mradi huu nao pia utahakikisha maji yanafika kwenye eneo la kituo cha afya ambacho kinajengwa kwenye Kata ile ya Rabour?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Chege kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, mkakati wa Serikali ni kuhakikisha vijiji vyote vinafikiwa na maji ya bomba yaliyo safi na salama yakiwa ya kutosha. Hivyo niombe Mheshimiwa Mbunge tuendelee kushirikiana, vijiji hivi vyote vitapata maji.

Mheshimiwa Spika, swali la pili, kuhusiana na kituo cha afya, nimekuwa nikiongea hapa mara nyingi, tumeshaelekeza watendaji wetu kwenye mikoa yote na wilaya zote kuhakikisha maeneo yote yanayotoa huduma za afya, kwa maana ya vituo vya afya, zahanati hospitali yote yanakuwa na mitandao ya maji safi na salama ya kutosha. Lakini vilevile eneo lake Mheshimiwa Chege nalo ni moja ya maeneo ambayo tunakwenda kuyafanyia kazi na kituo cha afya nacho ni miongoni mwa vituo vitakavyoenda kunufaika.

Name

Esther Lukago Midimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JAFARI W. CHEGE aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka mradi wa maji safi na salama katika Kata ya Rabour?

Supplementary Question 2

MHE. ESTHER L. MIDIMU: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza swali la nyongeza.

Je, ni lini Serikali itachimba visima vya maji katika Kata ya Mwabazuru, Budekwa na Busiriri Wilaya ya Maswa?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Esther, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, awali ya yote nipende kumpongeza sana Mheshimiwa Esther, amekuwa akifuatilia hivi visima.

Mheshimiwa Spika, mpango wa Serikali ni kuhakikisha maeneo haya yanayohitaji huduma ya maji kupitia visima yanafikiwa, hivyo hata Wilaya ya Magu nayo ni miongoni mwa wilaya ambazo tunakwenda kuzifikia. Mwaka ujao wa fedha tuna visima vya kutosha tulivyovitenga katika bajeti yetu, hivyo tutahakikisha kwamba Magu nao wanapata.