Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 24 Water and Irrigation Wizara ya Maji 209 2022-05-17

Name

Jafari Chege Wambura

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rorya

Primary Question

MHE. JAFARI W. CHEGE aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka mradi wa maji safi na salama katika Kata ya Rabour?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maji naomba kujibu swali la Mheshimiwa Jafari Wambura Chege Mbunge wa Rorya kama ifuatavyo: -

Mheshimwa Spika, Kata ya Rabour ina jumla ya Vijiji vitatu vya Oliyo, Rabour na Makongoro. Vijiji vya Oliyo na Rabour vinapata huduma ya maji kupitia visima virefu. Katika kuboresha huduma ya maji katika Kata ya Rabour (Kijiji cha Rabour), Serikali katika mwaka wa fedha 2021/2022 inatekeleza mradi wa maji katika kijiji hicho. Kazi zilizopangwa kutekelezwa ni ujenzi wa tenki lenye ujazo wa lita 225,000 na ujenzi wa mtandao wa usambazaji maji wenye urefu wa kilometa 12.8. Mradi huu unatarajiwa kukamilika mwishoni mwa mwezi Juni, 2022 na utanufaisha wananchi wapatao 4,792.

Mheshimwa Spika, katika mwaka wa fedha 2022/2023 Serikali itaendelea na utekelezaji wa miradi ya maji katika Vijiji viwili vya Oliyo na Makongoro. Kukamilika kwa miradi hiyo kutaboresha huduma ya maji safi na salama katika Kata yote ya Rabour.