Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Anastazia James Wambura

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANASTAZIA J. WAMBURA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Kituo cha Afya katika Kata ya Mangopacha Nne ili kuwanusuru Akina Mama na tatizo la ukosefu wa huduma wakati wa kujifungua?

Supplementary Question 1

MHE. ANASTAZIA J. WAMBURA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali moja la nyongeza. Kwanza nishukuru sana majibu ya Mheshimiwa Waziri, na nimpongeze, huwa anatembelea sana Mkoa wa Mtwara.

Mheshimiwa Spika, ninakiri hizo fedha milioni 250 kwa ajili ya Kituo cha Afya cha Mkunwa, zimefika na zinaendelea kufanya kazi.

Mheshimiwa Spika, nimpe taarifa Mheshimiwa Waziri kwamba wananchi wa Mangopacha Nne, tayari walishaandaa eneo kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha afya muda mrefu tu, zaidi ya miaka mitano. Kwa hiyo, niombe sasa Serikali itoe kipaumbele fedha zitakapopatikana.

Mheshimiwa Spika, hii Kata ya Mangopacha Nne ni moja ya kata katika Tarafa ya Dihimba, ambapo tarafa hii haina hata kituo kimoja cha afya lakini kuna zahanati katika baadhi ya vijiji. Kuna tatizo kubwa sana la wanawake…

SPIKA: Swali lako Mheshimiwa.

MHE. ANASTAZIA J. WAMBURA: Mheshimiwa Spika, nauliza swali, katika kutatua tatizo la wanawake kujifungua hasa nyakati za usiku. Je, Serikali itakuwa tayari kuboresha huduma katika hizi zahanati ili kusudi akina mama waweze kupata huduma bora?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Anastazia James Wambura, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ninatambua kwamba anafanya kazi nzuri kwa Mkoa wa Mtwara na ndiyo maana amekuwa akitetea sana katika huduma za afya, hususan wanawake katika mkoa wake. Nimhakikishie tu kwamba Serikali ipo tayari kuboresha huduma katika tarafa hiyo, na tutalifanyia kazi, ahsante sana.

Name

Deodatus Philip Mwanyika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Njombe Mjini

Primary Question

MHE. ANASTAZIA J. WAMBURA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Kituo cha Afya katika Kata ya Mangopacha Nne ili kuwanusuru Akina Mama na tatizo la ukosefu wa huduma wakati wa kujifungua?

Supplementary Question 2

MHE. DEODATUS P. MWANYIKA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa wananchi wa Njombe walishakamilisha ujenzi wa vituo vya afya viwili kwenye Kata mbili, Kata ya Mamangolo na Kata ya Kifanya; na tumekuwa tukiomba sana hapa. Nini kauli ya Serikali kuhusu kutoa vifaa tiba kwenye hospitali ili mama mtoto aweze kupata huduma?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Deodatus Mwanyika, Mbunge wa Jimbo la Njombe Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, baada ya ukamilishaji wa vituo hivyo kinachofuatia ni kutafuta vifaa tiba na ambavyo vipo katika mpango. Kwa hiyo, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, tunanunua vifaa tiba kwa ajili ya vituo vya afya ambavyo vimeshakamilika. Vitakapokuwa vimepatikana tutavipeleka pale kwa wananchi, ahsante sana.