Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 24 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 207 2022-05-17

Name

Anastazia James Wambura

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANASTAZIA J. WAMBURA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itajenga Kituo cha Afya katika Kata ya Mangopacha Nne ili kuwanusuru Akina Mama na tatizo la ukosefu wa huduma wakati wa kujifungua?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Anastazia James Wambura, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2021/2022 Serikali imetoa fedha Shilingi bilioni 86 kwa ajili ya ujenzi wa vituo vya afya 234 kwenye kata za kimkakati kote nchini. Halmashauri ya Wilaya ya Mtwara imepokea Shilingi milioni 250 kwa ajili ya kuanza ujenzi wa Kituo cha Afya Mkunwa.

Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya kujenga vituo vya kutolea huduma za afya kwenye kata za kimkakati zenye uhitaji mkubwa ikiwa ni pamoja na ujenzi wa kituo cha afya kwenye Kata ya Mango Pacha Nne.