Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Abdulhafar Idrissa Juma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtoni

Primary Question

MHE. ABDUL-HAFAR IDRISSA JUMA K.n.y. MHE. USSI SALUM PONDEZA aliuliza: - Je, ni nchi ngapi zimeshafungua Ofisi zao za Ubalozi Jijini Dodoma baada ya zoezi la kuhamisha Makao Makuu ya Serikali Dodoma?

Supplementary Question 1

MHE. ABDUL-HAFAR IDRISSA JUMA: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri ya Serikali ningetamani pia kujua kwa niaba ya muuliza swali Je, ni Balozi ngapi ambazo walau zimeshakuwa na viwanja japokuwa hazijafungua ofisi rasmi kuelekea kuwa na Ofisi rasmi katika Makao Makuu ya nchi?

Mheshimiwa Spika, nashukuru. (Makofi)

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Balozi zote nchini zimegawiwa viwanja Dodoma na Taasisi zake na kila Ubalozi ulitengewa karibu heka tano tano kwa ajili ya kuwekeza makazi yake pale. (Makofi)

Name

Kunti Yusuph Majala

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ABDUL-HAFAR IDRISSA JUMA K.n.y. MHE. USSI SALUM PONDEZA aliuliza: - Je, ni nchi ngapi zimeshafungua Ofisi zao za Ubalozi Jijini Dodoma baada ya zoezi la kuhamisha Makao Makuu ya Serikali Dodoma?

Supplementary Question 2

MHE. KUNTI Y. MAJALA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa swali. Mheshimiwa Waziri ametuambia kwamba Balozi zote nchini zimepewa viwanja Dodoma.

Je, ni changamoto gani kubwa inayosababisha Balozi hizi zishindwe kuja kuendeleza viwanja hivyo na kuhamia Dodoma? (Makofi)

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kunti kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza utaratibu wa kuhamisha makazi ya Kibalozi kutoka iliyokuwa makao makuu ya nchi yetu kuja Dodoma ni utaratibu sawa na nchi nyingine zilivyofanya wakati huo. Kwa mfano, sisi tulihama kutoka Borne kwenda Berlin lakini tulichukua muda mrefu sana kwa sababu, hili ni suala la mipango ya kila nchi kujiwekea mpango wa uhamisho ambao unahitaji fedha. Kwa hiyo, upo uwezekano kabisa mkubwa wa nchi hizi ku-delay kuhamia hapa Dodoma kwa sababu, lazima ziingie kwenye mipango yao ya fedha na ziruhusu katika utaratibu wa kawaida Balozi zao kuhamishia makazi yake hapa makao makuu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini sambamba na hilo tukumbuke wakati tunafanya mchakato wa uhamisho baadhi ya Balozi zetu hapa ambazo zinawakilisha nchi zao hapa ndio zilikuwa zinamaliza majengo yao mapya Dar es Salaam. Kwa hiyo, unaweza ukaona namna ambavyo kunakuwa na misukosuko ile ya kimaandalizi kuanza kufikiria upya kuhamia Dodoma, ahsante. (Makofi)