Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Vita Rashid Kawawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Primary Question

MHE. VITA R. KAWAWA aliuliza: - Je, mpango wa ujenzi wa reli ya Kusini kutoka Mtwara hadi Ruvuma na matawi yake ya Liganga na Mchuchuma umefikia wapi?

Supplementary Question 1

MHE. VITA R. KAWAWA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa kuwa mradi huu upo katika mpango wa maendeleo ya miaka mitano. Je, Serikali inaweza kuona kuwa kuna haja sasa ya kuharakisha upatikanaji wa huyo Mwekezaji. Pia kufanya mazungumzo makini ili mradi huo uweze kuanza kwa haraka kwa muda uliokusudiwa? (Makofi)

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwanza napenda kujibu swali la Mheshimiwa Rashid Kawawa Mbunge wa Namtumbo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Mbunge anataka kujua kuharakisha mazungumzo ambayo yanaendelea kwa ajili ya mradi huu wa Liganga na Mchuchuma. Ni kweli majadiliano yameendelea na bahati nzuri sana nikuhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba majadiliano yako katika hatua za mwisho kabisa ili mradi huu uanze utekelezaji wake. Na kwa maana hiyo mara tu mazungumzo yatakapokamilika na sisi upande wa TRC kwa kuwa tayari fedha kutoka Umoja wa SADC wametuahidi kutoa hizo Dola 6,000,000 na sisi tutaanza utekelezaji wa mradi huu kwa ujenzi wa standard gauge.

Mheshimiwa Spika, swali lake la pili anataka kufahamu kwamba ni lini sasa mradi huu utaanza. Nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba mara tu mazungumzo yatakapokamilika mradi huu tutaanza utekelezaji wake. (Makofi)