Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 23 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 205 2022-05-16

Name

Vita Rashid Kawawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Primary Question

MHE. VITA R. KAWAWA aliuliza: -

Je, mpango wa ujenzi wa reli ya Kusini kutoka Mtwara hadi Ruvuma na matawi yake ya Liganga na Mchuchuma umefikia wapi?

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Vita Rashid Kawawa, Mbunge wa Namtumbo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Shirika la Reli Tanzania (TRC) imekamilisha kazi ya upembuzi na usanifu wa awali kwa ajili ya ujenzi wa njia ya reli ya Mtwara-Mbambabay na matawi yake ya Liganga na Mchuchuma kilomita 1,000. Upembuzi uliofanyika ulipendekeza kuwa utekelezaji wa mradi huo ushirikishe sekta binafsi. Kwa sasa Serikali inaendelea na taratibu za kumwajiri Mshauri Elekezi (Transaction Advisor) kwa ajili ya kuandaa Andiko, makabrasha ya zabuni ili kumpata mwekezaji kwa utaratibu wa ubia baina ya Sekta ya Umma na Binafsi (PPP).

Mheshimiwa Spika, aidha Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika -SADC imeahidi kutoa kiasi cha Dola za Marekani 6,000,000 kwa lengo la kumgharamia Mshauri Elekezi. Utaratibu wa kupata fedha hizi unaendelea na kazi hii inatarajiwa kufanyika Mwaka wa Fedha 2022/2023, ahsante.