Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Yustina Arcadius Rahhi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. YUSTINA A. RAHHI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Barabara za Dareda – Dongobesh, Katesh – Haydom, Karatu – Mbulu – Haydom – Singida na Babati hadi Orkesumet kama ilivyoainishwa katika Ilani ya Chama cha Mapinduzi ya mwaka 2020 – 2025?

Supplementary Question 1

MHE. YUSTINA A. RAHHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana, naishukuru pia Serikali kwa majibu mazuri lakini nina maswali mawili madogo ya nyongeza. Kwanza, naipongeza Serikali kwa barabara ya Karatu – Mbulu – Hydom, kipande kinachoanza Mbulu Garbab, kipande cha kilomita 25 taratibu za manunuzi zimeanza tangu Mei, 2021 na hadi sasa haujakamilika. Sasa wananchi wa Mbulu hamu yao ni kuona kwamba barabara hiyo inajengwa.

Je, ni lini taratibu hizo zitakamilika na ujenzi huo uanze?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili, barabara hizi nilizozitaja, Barabara ya Dareda, Dongobesh, Kartesh Hydom, Babati Orkesumet kupitia Galapo ni ahadi ya Serikali kwa wananchi wa Manyara ya muda mrefu. Lakini vile vile ni ahadi ya viongozi wa Serikali wakati wa kampeni. Ni barabara ambazo ziko kwenye Ilani ya Chama.

Sasa, ni lini Serikali itaanza rasmi ujenzi wa barabara hizo? Ahsante sana.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwanza nianze kwa kumpongeza sana Mheshimiwa Yustina Arcadius Rahhi kwa jinsi anavyosaidiana na Wabunge mbalimbali wa Mkoa wa Manyara ambao barabara hizi zinapita kwenye Majimbo yao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ametaja karibu barabara za mkoa mzima wa Manyara. Mimi nataka nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kipande alichokitaja kwenye swali lake la kwanza la Mbulu Garbab zabuni ilishatangazwa na sasa hivi tuko kwenye hatua ya kusaini mkataba; kwa hiyo siyo hadithi tena.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kipande cha pili cha Garbab Muslur tayari tumeshandaa zabuni na inatangazwa muda wowote. Kwa hiyo tutahakikisha kwamba kipande hiki cha kilomita 50 kati ya Mbulu na Hydom kitajengwa. Kwa barabara zingine alizozitaja ya Hydom - Katesh tayari tulishafanya usanifu wa awali na tunaendelea usanifu wa kina. Dongobesh – Dareda tayari tumeshakamilisha usanifu wa kina.

Vilevile Babati kwenda Galapo hadi Orkesmet barabara hii tunaendelea kuifanyia usanifu ili sasa tuweze kuijenga kwa kiwango cha lami.

Kwa hiyo nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge na Waheshimiwa wa Mkoa wa Manyara kwamba Serikali iliahidi na hatua zinaendelea kufanyika kuhakikisha kwamba ahadi zinatekelezwa kama zilivyo kwenye Ilani, lakini pia tunajenga hizo barabara kwa kiwango cha lami. Ahsante.

Name

Agnes Mathew Marwa

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. YUSTINA A. RAHHI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Barabara za Dareda – Dongobesh, Katesh – Haydom, Karatu – Mbulu – Haydom – Singida na Babati hadi Orkesumet kama ilivyoainishwa katika Ilani ya Chama cha Mapinduzi ya mwaka 2020 – 2025?

Supplementary Question 2

MHE. AGNES M. MARWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wilaya ya Rorya ni kati ya wilaya ambazo ziko nyuma sana kimaendeleo kutokana na changamoto ya miundombinu. Sasa;

je Serikali haioni kuna ulazima wa kuanza ujenzi wa barabara inayopita Mika, Utegi, Shirati hadi Kirongo; ukizingatia ni muda mrefu sasa, tangu 2017, 2018 ikiwa inafanyiwa upembuzi yakinifu?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Agnes Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Mara kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli barabara aliyoitaja inayoanzia Utegi katika Jimbo la Rorya ipo kwenye mpango wa kufanyiwa usanifu ili ikishafanyiwa usanifu tujue gharama halafu Serikali kama ilivyo kwenye Ilani tuweze kupata gharama na tuanze kuijenga kwa kiwango cha lami. Ahsante.

Name

Oran Manase Njeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbeya Vijijini

Primary Question

MHE. YUSTINA A. RAHHI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Barabara za Dareda – Dongobesh, Katesh – Haydom, Karatu – Mbulu – Haydom – Singida na Babati hadi Orkesumet kama ilivyoainishwa katika Ilani ya Chama cha Mapinduzi ya mwaka 2020 – 2025?

Supplementary Question 3

MHE. ORAN M. NJEZA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana. Kwa kuwa barabara ya Ishonje, Kikondo kuelekea Makete kwa muda mrefu sasa imekuweko kwenye bajeti ya kujengwa kwa kiwango cha lami.

Je, ni lini sasa hiyo barabara, hususan kipande cha Ishodye, Kikondo kuelekea Makete, itajengwa kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Oran Njeza Mbunge wa Mbeya Vijijini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekitti, Barabara aliyoitaja ya Ishonje Kikonde Makete ilitangazwa kilomita kama 25 haikupata mkandarasi. Lakini imetangazwa tena ambapo sasa tumeongeza hata kilometa siyo tena 25 ni kilomita kama 50, na ni mwendelezo wa barabara ya kutoka Njombe, Makete kuja Ishondye ambayo inaunganisha mkoa wa Mbeya na mkoa wa Njombe. Kwa hiyo nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tayari barabara hii imeshatangazwa na ni taratibu tu za manunuzi ambapo tutaanza kuanzia Makete kuendeleza kwenda kuunganisha na mkoa wa Mbeya. Ahsante.

Name

Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. YUSTINA A. RAHHI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Barabara za Dareda – Dongobesh, Katesh – Haydom, Karatu – Mbulu – Haydom – Singida na Babati hadi Orkesumet kama ilivyoainishwa katika Ilani ya Chama cha Mapinduzi ya mwaka 2020 – 2025?

Supplementary Question 4

DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipatia nafasi kuuliza swali dogo. Barabara ya kuanzia Kilosa, Lumuma Mpwapwa Ulering’ombe mpaka Ruaha ni mbovu sana.

Je, ni lini angalau itafanyiwa ukarabati kwa kiwango cha changarawe? Ahsante.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Ishengoma Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Barabara zote za TANROADS zinatengenezwa kwa kiwango cha changarawe. Kwa hiyo nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba barabara hiyo katika mwaka huu wa fedha tutahakikisha kwamba tunaitengeneza kama kuna sehemu ina udongo tutahakikisha kwamba tunapeleka fedha ili tuweze kutengeneza barabara hiyo kwa kiwango cha changarawe ili iweze kupitika muda wowote ili kutoa huduma bora kwa wananchi wahusika, ahsante. (Makofi)

Name

Neema Gerald Mwandabila

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. YUSTINA A. RAHHI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Barabara za Dareda – Dongobesh, Katesh – Haydom, Karatu – Mbulu – Haydom – Singida na Babati hadi Orkesumet kama ilivyoainishwa katika Ilani ya Chama cha Mapinduzi ya mwaka 2020 – 2025?

Supplementary Question 5

MHE. NEEMA G. MWANDABILA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Katika Wilaya ya Ileje hivi karibuni tumeona namna gani maafa yamekuwa yakitokea kutokana na maporomoko yanayotokea katika barabara ya Ikuti, Sange, Katengele, Kafule mpaka Ikinga. Nilitamani kufahamu ni nini mkakati wa Serikali kuhakikisha barabara hizi zinajengwa kwa kiwango cha lami? Ahsante.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Neema Mwandabila, Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Songwe kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli barabara alizozitaja za kuanzia Isongole, Ibungu, Katengele hadi Kimo ambayo inaunganisha Ileje na Wilaya ya Rungwe; lakini pia barabara za Isongole, Ibungu, Malangali, Ikinga hadi Kasumulu zinazounganisha Wilaya ya Ileje na Kyela ni barabara ambazo zinapita kwenye miinuko na ni kweli kulitokea maporomoko makubwa sasa mimi mwenyewe nilienda kwasababu zilikuwa zimefunga.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa kinachoendelea sasa hivi ni kwamba ni kuzifanyia usanifu wa kina barabara ya Isongole, Ibungu, Malangali, Ikinga hadi Kasumulu ili kufanya maandalizi kwa ajili ya kuijenga kwa kiwango cha lami. Lakini hatua ambazo zimechukuliwa kwa sasa ni kuondoa vile vifusi ili barabara ziweze kufunguka maana yake zilikuwa zimefungwa na nisema tu katika haya maporomoko tulipoteza watu watano baada ya kutokea land slide kwa hiyo unaweza ukaona lakini barabara ya kutoka Ibungu kwenda Tukuyu tutaainisha maeneo korofi ili yaweze kufanyiwa matengenezo maalum na barabara hiyo iweze kupitika kwa kipindi chote cha mwaka, ahsante. (Makofi)