Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 22 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 195 2022-05-13

Name

Yustina Arcadius Rahhi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. YUSTINA A. RAHHI aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Barabara za Dareda – Dongobesh, Katesh – Haydom, Karatu – Mbulu – Haydom – Singida na Babati hadi Orkesumet kama ilivyoainishwa katika Ilani ya Chama cha Mapinduzi ya mwaka 2020 – 2025?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi napenda kujibu swali la Mheshimiwa Yustina Arcadius Rahhi, Mbunge Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeanza maandalizi kwa ajili ya ujenzi kwa kiwango cha lami wa Barabara za Dareda – Dongobesh (km 60), Katesh – Hydom (km 70), Karatu
– Mbulu – Hydom – Singida (km 246) na Babati - Orkesumet (km 145). Kwa kipande cha Mbulu – Garbab chenye urefu wa kilometa 25, taratibu za zabuni ziko kwenye hatua za mwisho za kusaini mkataba. Kwa kipande cha kutoka Garbab – Muslur chenye urefu wa kilometa 25 maandalizi ya kutangaza zabuni kwa ajili ya kumpata mkandarasi wa ujenzi yako kwenye hatua za mwisho. Aidha, Serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya ujenzi wa sehemu zilizobaki. Ahsante.