Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Josephine Johnson Genzabuke

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

Pori la Akiba la Kagera Nkanda lililopo Wilaya ya Kasulu lilianzishwa kipindi ambacho Wilaya ya Kasulu ilikuwa na wakazi wachache na kwa sasa idadi ya watu katika Wilaya hiyo imekuwa kubwa na kufanya mahitaji ya ardhi kuwa makubwa, pia hivyo kusababisha mgogoro baina ya wakulima na wafugaji na mamlaka za misitu na wanyaa pori. Je, Serikali imejipanga vipi kumaliza migogoro hii na kuwasaidia wananchi?

Supplementary Question 1

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Naibu Spika nakushukuru kwa kunipa nafasi ili niulize swali la nyongeza, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa ni muda ni muda mrefu sana mgogoro wa Kagera Nkanda umekuwa ukiongelewa humu Bungeni lakini maka sasa hakuna ufumbuzi ambao umeshapatikana. Na kwa kuwa watu wanaongezeka lakini ardhi haiongezeki, ni lini Serikali italeta sheria Bungeni ili ifanyiwe marekebisho kusudi mipaka iweze kusogezwa wananchi wapate maeneo ya kulima?

Name

Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nitoe taarifa tu kwamba ni kweli migogoro inayohusisha mipaka kwenye hifadhi iwe hifadhi za misitu na hifadhi za wanyamapori ni mikubwa na ni kweli sasa imekuwepo kwa muda mrefu. Lakini napenda tu nitoe taarifa kwamba kama nilivyojibu kwenye swali langu la msingi sasa tunakwenda kupata ufumbuzi wa matatizo haya, tutapiga hatua na kuweza kuyapunguza matatizo haya kama sio kuyamaliza baada ya zoezi tunalolitaja ambalo litashirikisha Wizara sita kwenda kuangalia hasa uhalisia wa matatizo kwenye mipaka hii.
Mheshimiwa Naibu Spika, nimesema awali na isichukuliwe kwamba utatuzi au ufumbuzi wa changamoto za ardhi iko kwenye hifadhi za taifa peke yake, hapana, ndiyo maana tunasema sasa tunakwenda kwa ujumla wetu Wizara sita zote ambazo ni watumiaji wa ardhi ili tuweze kwenda kubaini kwamba ni kweli kuna uhaba wa ardhi au kuna matatizo mengine yanayosababisha watu kuingia kwenye hifadhi? Kwa hiyo, tutakwenda kuchakata na kuangalia mahitaji yapi ya ardhi yanahitaji ardhi ambayo tunaweza kuipata wapi kabla hatujaingia kwenye hifadhi ambako kumezuiliwa kwa mujibu wa sheria.

Name

Joseph Kasheku Musukuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita

Primary Question

Pori la Akiba la Kagera Nkanda lililopo Wilaya ya Kasulu lilianzishwa kipindi ambacho Wilaya ya Kasulu ilikuwa na wakazi wachache na kwa sasa idadi ya watu katika Wilaya hiyo imekuwa kubwa na kufanya mahitaji ya ardhi kuwa makubwa, pia hivyo kusababisha mgogoro baina ya wakulima na wafugaji na mamlaka za misitu na wanyaa pori. Je, Serikali imejipanga vipi kumaliza migogoro hii na kuwasaidia wananchi?

Supplementary Question 2

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kuniona.
Kwa kuwa tatizo lililopo Kagera ni sawasawa na tatizo lililopo kwenye Jimbo la Geita Vijijini katika Msitu wa Lwande. Sisi kama Halmashauri tulipendekeza hekta 7,000 zirudishwe kwa wananchi kutoka kwenye hekta 15,000; na tukapeleka maombi yetu Wizarani. Je, ni lini Serikali itajibu maombi ya Wilaya yetu kuhusiana na hizo hekta 7000?

Name

Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, nimetoa maelezo ya awali ambayo napenda niyasisitize tena; hakuna jambo zuri katika kushughulikia changamoto yoyote ile kama kufanya utafiti, kama kwenda kutafuta kiini cha tatizo, usipofanya hivyo ukatafuta suluhisho utafuta suluhisho pengine ukapata suluhisho la muda tu. Lakini ukitaka suluhisho la kudumu lazima ufanye utafiti, kama vile ambavyo ukiwa na maradhi unataka kutibiwa unakwenda kwanza maabara unafanya vipimo.
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa tumesema tunataka kwenda kwenye maeneo haya yote kwa ujumla wake ikiwemo kwenye eneo ambalo Mheshimiwa Joseph Musukuma analizungumzia. Napenda nimuombe Mheshimiwa Musukuma avute subira kidogo; maombi aliyopeleka Wizara ya Maliasili na Utalii hayatashugulikiwa na Maliasili tu peke yake. Tumesema tunakwenda kushirikisha Wizara zote ambazo ni wasimamizi au ni watumiaji wa ardhi ikiwemo TAMISEMI ambayo wamesema kwamba wamepitisha maombi kule, tunakwenda kushirikiana nao kwenda kutafuta ufumbuzi ambao utauwa ufumbuzi wa kudumu.

Name

Kasuku Samson Bilago

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Buyungu

Primary Question

Pori la Akiba la Kagera Nkanda lililopo Wilaya ya Kasulu lilianzishwa kipindi ambacho Wilaya ya Kasulu ilikuwa na wakazi wachache na kwa sasa idadi ya watu katika Wilaya hiyo imekuwa kubwa na kufanya mahitaji ya ardhi kuwa makubwa, pia hivyo kusababisha mgogoro baina ya wakulima na wafugaji na mamlaka za misitu na wanyaa pori. Je, Serikali imejipanga vipi kumaliza migogoro hii na kuwasaidia wananchi?

Supplementary Question 3

MHE. KASUKU S. BILAGO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana.
Mgogoro uliopo Kasulu - Kagera Nkanda unafanana kabisa na mgogoro ambao upo Wilaya ya Kakonko ambako tunayo mbuga ya wanayama ya Moyowosi na Kigosi inayozungumzwa. Vijiji vya Mganza, Itumbiko, Kabingo na Kanyonza vinapakana na maeneo hayo na; kwa hiyo vimekosa ardhi kabisa ya kutumia kwasababu ya ongezeko la watu. Kwa hiyo, nauliza swali; ni lini mchakato huo wa Wizara ya Maliasili na Utalii itaiona hoja ya wananchi kuongezewa ardhi kutoka kwenye hifadhi badala ya hifadhi kuwa na ardhi kubwa kuliko wananchi? Ahsante.

Name

Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, kimsingi maswali yote yanayohusiana na migogoro ya mipaka ambayo unaweza ukaiita migogoro ya ardhi, lakini inayohusiana na hifadhi yanakuwa yanahusiana na maliasili na utalii. Ukizungumzia migogoro ya ardhi hiyo hoja ni pana zaidi kuliko hivi sasa.
Kwa hiyo, suala ni lini tutashugulikia mgogoro wa Kakonko kule jibu ni lile lile, kwamba tuvute subira tusubiri twende tufike kwenye maeneo haya tufanye utafiti, tufanye ukaguzi ili twende tukafanye team work.
Mheshimiwa Naibu Spika, bila kwenda kukagua kwa pamoja tukaangalia pengine tunaweza tukakurupuka na majawabu ambayo si sahihi. Ipeni nafasi Serikali tufike kule, Wizara zote sita kwa ujumla wetu tukishirikisha TAMISEMI lakini pia tukishirikisha hata wananchi wenyewe ambao ndio wanaguswa na matatizo na changamoto hizi. Zoezi zima litakuwa ni shirikishi, kwa hiyo tutapata majawabu ambayo yatakuwa ni ya kudumu.

Name

Alex Raphael Gashaza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngara

Primary Question

Pori la Akiba la Kagera Nkanda lililopo Wilaya ya Kasulu lilianzishwa kipindi ambacho Wilaya ya Kasulu ilikuwa na wakazi wachache na kwa sasa idadi ya watu katika Wilaya hiyo imekuwa kubwa na kufanya mahitaji ya ardhi kuwa makubwa, pia hivyo kusababisha mgogoro baina ya wakulima na wafugaji na mamlaka za misitu na wanyaa pori. Je, Serikali imejipanga vipi kumaliza migogoro hii na kuwasaidia wananchi?

Supplementary Question 4

MHE. ALEX R. GASHAZA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi hii niweze kuuliza swali la nyongeza.
Kwa kuwa mgogoro uliopo katika Pori la Kagera Nkanda unataka kufanana na matatizo yaliyopo katika Pori la Burigi na Kimisi hususan maeneo yaliyopo katika Jimbo la Ngara; kama ambavyo tangu mkutano wa pili wa Bunge niliweza kueleza na hata katika mchango wangu wa bajeti ya maliasili; kwamba tangu mwaka 1959 mrahaba ule wa asilimia 25 ambao unatakiwa kurudishwa kwenye Halmashauri kutokana na vitalu vya uwindaji haijawahi kupelekwa kwenye Jimbo la Ngara.
Mheshimiwa Naibu Spika, je, Waziri wa Maliasili na Utalii anaweza kuwaeleza wananchi wa Jimbo la Ngara na Halmashauri ya Wilaya ya Ngara, ni lini pesa hizo zitapelekwa, ambazo tangu mwaka 1959 mpaka leo hazijapelekwa?

Name

Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, swali la mrabaha likilinganishwa na swali la msingi ambalo nimelijibu ni mahususi kidogo na bila shaka linahitaji takwimu na linahitaji taarifa ambayo ni mahususi.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini nimuahidi Mheshimiwa Mbunge baada ya kipindi hiki cha asubuhi, mchana awasiliane na mimi nitaweza kumpa jibu sahihi kwa swali lake ambalo ni mahususi.