Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

John Michael Sallu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Handeni Vijijini

Primary Question

MHE. JOHN M. SALLU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga daraja la Kwasunga – Handeni Vijijini?

Supplementary Question 1

MHE. JOHN M. SALLU: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali moja la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa barabara ya Sindeni – Kwedikwazu ni barabara muhimu na kuna idadi kubwa ya watu na vilevile inatumika kutoa mazao mengi; na kipindi cha mvua inasumbua sana. Je, ni lini Serikali itaitengeneza barabara hiyo kwa kiwango cha lami?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa John Marko Saluu, Mbunge wa Jimbo la Handeni Vijijini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kwamba Serikali ina mpango wa kuhakikisha barabara zile zenye shida kutafuta fedha ili tuzitengee na kuzijenga kwa kiwango cha lami. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge najua anafanya kazi nzuri ya kuwatetea wananchi wake katika Jimbo la Handeni Vijijini, kwa hiyo katika hilo nimwambie tu kwamba kadri tutakavyopata fedha basi eneo lake tutalizingatia sana.