Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 20 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 174 2022-05-11

Name

John Michael Sallu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Handeni Vijijini

Primary Question

MHE. JOHN M. SALLU aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itajenga daraja la Kwasunga – Handeni Vijijini?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-TAMISEMI, naomba kujibu Swali la Mheshimiwa John Marko Sallu Mbunge wa Jimbo la Handeni Vijijini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Wilaya ya Handeni na Wilaya ya Bagamoyo inatenganishwa na Mto Mligazi. Mto huu umekuwa changamoto kubwa kwa watumiaji wa barabara ya Kwasunga inayotoka Mkata kuelekea Kwasunga kuunganisha vijijni vya Miyono katika Wilaya ya Bagamoyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika bajeti ya mwaka wa fedha 2021/2022 TARURA Mkoa wa Tanga imeingia mkataba Na. AE/092/2021-2022/TAG/C/01 na Mkandarasi Mshauri kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kupitia Kampuni ya BICO wenye gharama ya Shilingi milioni 42.98 kwa ajili ya uchunguzi wa miamba. Kazi ya uchunguzi imeshafanyika na kwa sasa mkandarasi huyo yupo katika hatua ya mwisho ya kuwasilisha taarifa ya matokeo ya uchunguzi ambapo baada ya kazi ya usanifu wa daraja pamoja na uandaaji wa michoro na gharama za ujenzi Serikali itatenga fedha za ujenzi wa daraja hilo.