Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Innocent Edward Kalogeris

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini

Primary Question

MHE. INNOCENT E. KALOGERIS aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya kujenga vyumba vinne vya madarasa na bweni katika Shule ya Sekondari Matombo Kata ya Konde?

Supplementary Question 1

MHE. INNOCENT E. KALOGERIS: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa majibu mazuri sana ya Serikali, nina maswali mawili ya nyongeza.

La kwanza; uhitaji wa vyumba vya madarasa na mabweni katika shule za sekondari ambazo ziko pembezoni katika Halmashauri ya Morogoro Vijijini ni mkubwa kama vile Shule ya Sekondari Kasanga, Bwakila Juu na Singisa.

Je, Serikali ina mpango gani wa kuwasaidia wananchi wa Morogoro Vijijini katika kata tajwa katika ujenzi wa vyumba vya madarasa na mabweni ili kuwaondolea wanafunzi adha ya kutembea mwendo mrefu, lakini vilevile msongamano darasani?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kuona ni kuamini; je, Mheshimiwa Waziri yupo tayari kuongozana na mimi kwenda katika kata tajwa ili kujionea kwa uhalisi tatizo kubwa tulilokuwa nalo na kuweza kutusaidia?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Innocent Edward Kalogeris, Mbunge wa Morogoro Kusini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba mpango wa Serikali ni kuhakikisha kata zote za pembezoni tunazifikia kwa kujenga shule, lakini vilevile kwa kuongeza madarasa.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, nimuondoe hofu Mheshimiwa Mbunge kwamba kata hizo tutazifikia, na mimi niseme tu kwamba nitakwenda na nitaongozana naye kwenda kushuhudia katika hayo maeneo. (Makofi)

Name

Selemani Moshi Kakoso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Vijijini

Primary Question

MHE. INNOCENT E. KALOGERIS aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya kujenga vyumba vinne vya madarasa na bweni katika Shule ya Sekondari Matombo Kata ya Konde?

Supplementary Question 2

MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika ni miongoni mwa halmashauri zilizopata fedha nyingi za Serikali kwaajili ya ujenzi wa madarasa; je, Serikali ina mpango gani mkakati wa kuongeza mabweni kwenye Shule za Sekondari za Bulamata, Kakoso na Kabungu?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana na naomba kujibu swali la Mheshimiwa Kakoso, Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kwamba, katika maeneo ya Tanganyika ambayo Mheshimiwa Mbunge ameainisha nimhakikishie tu kwamba Serikali ni kuhakikisha na yenyewe tunayafikia; na ndiyo maana sasa hivi tuna programu mbalimbali kuwafikia katika maeneo ambayo hayafikiki. Kwa hiyo, nimuondoe hofu kwenye hili analolizungumza. Ahsante.

Name

Saashisha Elinikyo Mafuwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hai

Primary Question

MHE. INNOCENT E. KALOGERIS aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya kujenga vyumba vinne vya madarasa na bweni katika Shule ya Sekondari Matombo Kata ya Konde?

Supplementary Question 3

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, Wilaya ya Hai ina shule 13 chakavu sana na Mheshimiwa Rais alipotembelea Wilaya ya Hai, aliahidi kutupa fedha kwa ajili ya kujenga maboma ya shule hizi chakavu, lakini wewe mwenyewe Mheshimiwa Naibu Waziri pia ametembele Wilaya ya Hai na amejionea shule zilivyo chakavu. Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya Mheshimiwa Rais?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Saashisha Mafuwe, Mbunge wa Jimbo la Hai kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, nimuondoe wasiwasi, kwamba mpango wa Serikali wa marekebisho ya shule tutaanza katika mwaka wa fedha wa 2022/2023. Najua moja ya shule niliahidi ni Makeresho na ipo katika huo mpango, ahsante sana.

Name

Dr. Christina Christopher Mnzava

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. INNOCENT E. KALOGERIS aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya kujenga vyumba vinne vya madarasa na bweni katika Shule ya Sekondari Matombo Kata ya Konde?

Supplementary Question 4

MHE. DKT. CHRISTINA C. MNZAVA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, kwa kuwa Serikali yetu ya Chama cha Mapinduzi imejitahidi kujenga shule za sekondari katika kila kata na kuna watoto wengi hasa wasichana wanatoka wanatembea kilometa zaidi ya tano; je, Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha kwamba shule zinakuwa na mabweni angalau kunusuru watoto wa kike na hawa fataki?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Mnzava, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, mpango wa Serikali ni kuhakikisha kwamba tunajenga shule na mabweni katika maeneo ya pembezoni hususani maeneo yale ya wafugaji zaidi kuhakikisha kwamba watoto wote wanapata ile huduma ya shule bila kwenda umbali mrefu. Kwa hiyo, hilo lipo katika mpango wa Serikali, ahsante.

NAIBU SPIKA: Haya katika mipango yako uweke vilevile na Kisutu Secondary School.

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Naibu Spika, sawasawa.

NAIBU SPIKA: Imeingia kwenye Hansard hiyo.

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Naibu Spika, imeingia hiyo.