Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 20 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 173 2022-05-11

Name

Innocent Edward Kalogeris

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini

Primary Question

MHE. INNOCENT E. KALOGERIS aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya kujenga vyumba vinne vya madarasa na bweni katika Shule ya Sekondari Matombo Kata ya Konde?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Innocent Edward Kalogeris, Mbunge wa Morogoro kusini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Shule ya Sekondari Matombo iko katika Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro. Shule hii ni ya kidato cha kwanza hadi cha sita, hivyo, kutokana na ongezeko la wanafunzi wanaofaulu mtihani darasa la saba na kidato cha nne kila mwaka shule inahitaji miundombinu ya kutosha ikiwemo bweni na madarasa.

Mheshimiwa Naibu Spika, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais- TAMISEMI alitembelea na kuona hali halisi ya miundombinu ya Shule ya Sekondari Matombo tarehe 22 Septemba, 2021 na kuahidi kujenga madarasa manne na bweni moja mwaka wa fedha 2022/2023 kupitia programu zake mbalimbali ikiwemo SEQUIP na EP4R zinazojenga miundombinu ya elimu katika Mamlaka za Serikali za Mitaa.