Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Latifa Khamis Juwakali

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. LATIFA KHAMIS JUWAKALI aliuliza: - Je, ni vikundi vingapi vya vijana wa Zanzibar vimenufaika na mikopo au uwekezaji kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Vijana Taifa?

Supplementary Question 1

MHE. LATIFA KHAMIS JUWAKALI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza maswali mawili ya nyongeza na nimshukuru Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza; mfuko huu upo chini ya ofisi ya Waziri Mkuu, Serikali haioni haja sasa ya kuendelea kutoa fedha hizo kwa vijana wa Tanzania Bara na Tanzania Visiwani?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, je, mbali na mikopo kuna fursa nyingine zipi zinaweza kupatikana katika Ofisi ya Waziri Mkuu? Ahsante.

Name

Paschal Katambi Patrobas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shinyanga Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, VIJANA, AJIRA NA WENYE ULEMAVU (MHE. PASCAL P. KATAMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Latifa Khamis Juwakali kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kama nilivyojibu katika jibu langu la msingi la awali, suala hili linaongozwa kwa mujibu wa sheria ya fedha ambayo ni Sheria Namba 6 mwaka 2001, kwa masuala ambayo hayahusiana na Muungano. Lakini kwa kuwa tuna mashirikiano mazuri na upande wa Tanzania Zanzibar tutaendeleza ushirikiano huo katika masuala ya mafunzo kupeana fursa za mitaji na ajira kama jinsi ambavyo Wizara hizi zimekuwa zikishirikiana kwa karibu sana kwa kipindi chote.

Kwa hiyo, tutaendelea ushirikiano huo mzuri na tunashukuru kwa wazo hilo ambalo umelitoa na sisi tutalifanyia kazi tuone namna gani bora la kuweza kulirasimisha na pengine hata ikilazimisha kubadilisha sera au sheria tutalifanyia kazi. (Makofi)