Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 20 Youth, Disabled, Labor and Employment Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu 172 2022-05-11

Name

Latifa Khamis Juwakali

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. LATIFA KHAMIS JUWAKALI aliuliza: -

Je, ni vikundi vingapi vya vijana wa Zanzibar vimenufaika na mikopo au uwekezaji kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Vijana Taifa?

Name

Paschal Katambi Patrobas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shinyanga Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, VIJANA, AJIRA NA WENYE ULEMAVU (MHE. PASCAL P. KATAMBI) alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Latifa Khamis Juwakali kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Mfuko wa Maendeleo ya Vijana umeanzishwa kwa Sheria ya Fedha Namba 6 ya 2001 (The Public Finance Act, 2001) chini ya kifungu namba 45, ikisomwa sambamba na kifungu namba 12 cha sheria hiyo, ambapo Mfuko wa Maendeleo ya Vijana hutoa huduma ya mikopo yenye masharti nafuu kwa vijana Tanzania Bara tu.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa upande wa Zanzibar upo Mfuko wa Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi ambao pia unahudumia vijana na wana mpango maalum unaowahudumia vijana wa Zanzibar chini ya Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni, na Michezo na unaendeshwa kwa mujibu wa taratibu na sheria za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. Hivyo, kwa pande zote mbili za Muungano tuna ushirikiano wa karibu katika masuala yote ya maendeleo ya vijana na kubadilishana uzoefu, lakini pia masuala ya utatuzi wa changamoto kwa ajili ya kuwajenga vijana katika kuweza kupata fursa za ajira na mitaji. Ahsante.