Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Anton Albert Mwantona

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rungwe

Primary Question

MHE. ANTON A. MWANTONA aliuliza: - Je, ni lini mradi wa maji wa Tukuyu utakamilika?

Supplementary Question 1

MHE. ANTON A. MWANTONA: Mheshimiwa Spika, naomba kwanza nishukuru kwa majibu mazuri ya Wizara.

Mheshimiwa Spika, mradi unasuasua hauendi vizuri sana kwa sababu ni mwezi wa Nane sasa hivi hakuna kinachoendelea kule kwenye mradi, ukiuliza kwanini unasuasua wanatuambia kwamba ni kwa sababu unatekelezwa kwa force account na watumishi wapo busy na mambo mengine.

Je, Serikali ipo tayari kutafuta Mkandarasi badala ya kutumia force account ili mradi uweze kwenda haraka na wananchi wapate huduma ya maji? Ahsante.

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza na Mheshimiwa Mwantona kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, awali ya yote nipende kukupongeza kwa ufuatiliaji mzuri wa hili suala la maji la Tukuyu Mjini na hata jitihada ambazo zimefikiwa kwa kilometa tatu ni kwa sababu ya ushirikiano, hivyo ninapende kukuondoa hofu.

Mheshimiwa Spika, force account ni moja ya namna ambavyo inasaidia katika Wizara na miradi inakuwa vizuri, lakini suala la kuweka Mkandarasi kwa baadhi ya maeneo naomba tuseme tumeipokea na tutaweza kushauriana namna bora ya kulifanyia kazi. (Makofi)

Name

Josephine Johnson Genzabuke

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANTON A. MWANTONA aliuliza: - Je, ni lini mradi wa maji wa Tukuyu utakamilika?

Supplementary Question 2

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Katika Mji wa Kasulu maji yanayotoka kwenye mamomba ni machafu na yana tope, tulileta ombi hili ndani ya Bunge lako na Waziri akaahidi kumaliza tatizo hilo. Je, ni lini sasa tatizo hilo la maji katika Mji wa Kasulu litapatiwa majibu?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge wa Viti Maalum Kasulu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, maji machafu na tope; hii tunaendelea kufanyia kazi kuona tunajenga machujio, lakini vilevile kutumia dawa kutibu maji haya ili yaendelee kuwafikia wananchi yakiwa safi na salama.

Name

Mrisho Mashaka Gambo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arusha Mjini

Primary Question

MHE. ANTON A. MWANTONA aliuliza: - Je, ni lini mradi wa maji wa Tukuyu utakamilika?

Supplementary Question 3

MHE. MRISHO M. GAMBO: Mheshimiwa Spika, kwa kuwa changamoto iliyopo Rungwe inafanana na Mradi wa Maji katika Jiji la Arusha.

Je, Wizara ina mpango gani kuhangaika na changamoto ya malalamiko ya wananchi ya bill kubwa za maji?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mrisho Gambo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, bill kubwa za maji tunaendelea kulifanyia kazi kwa kutoa ushirikiano wa wasoma mita na mtumia maji, lakini vilevile tuna mfumo ambao tayari baadhi ya mikoa umeanza kutumika kuona kwamba unatumiwa message una hakiki kwamba ndicho ulichokitumia kisha unaletewa bill sasa ya malipo. Hivyo bill kubwa ukomo wake umeshafikia kwa sababu ya unified billing system.

Name

Iddi Kassim Iddi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Msalala

Primary Question

MHE. ANTON A. MWANTONA aliuliza: - Je, ni lini mradi wa maji wa Tukuyu utakamilika?

Supplementary Question 4

MHE. IDDI KASSIM IDDI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Nataka kumuuliza Naibu Waziri; Kata ya Mwanase, Mradi wa Maji wa Izuga umechukua muda mrefu sana. Sasa ni lini Serikali itapeleka fedha ya kuwalipa wakandarasi ili waweze kumaliza mradi huo wa maji wa Izuga?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

MHE. NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la Mheshimiwa Iddi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kupeleka fedha; tayari wakandarasi wanaendelea kulipwa, hivyo ninaamini hata mkandarasi huyu naye yupo kwenye foleni ya kulipwa. Tayari Katibu Mkuu pamoja na timu nzima inayohusika inaendelea kufanyia kazi suala hili la malipo.